Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya imeendelea kung’ara na kuvunja rekodi kwa kutoa wafanyakazi hodari kwa vipindi viwili (mwaka 2022 na 2024).
Hatua hii imefikiwa baada ya mfanyakazi hodari Joshua J. Kusaga, Fundi Sanifu vifaa tiba, kuchaguliwa kuwa mfanyakazi hodari Mei Mosi kitaifa.
Katika hafla iliyofanyika jijini Arusha, Joshua alikabidhiwa zawadi na Makamu wa Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango ambaye alikuwa Mgeni rasmi katika sherehe hizo.
Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya inajivunia kuwa na wafanyakazi wenye uwezo mkubwa na inaendelea kuweka msisitizo katika kutoa huduma bora za afya kwa wananchi. Mfanyakazi huyu ameonyesha uwezo, bidii na utaalamu wa hali ya juu katika kutekeleza majukumu yake.
Tunampongeza Joshua J. Kusaga kwa mafanikio haya makubwa na tunamtia moyo kuendelea kufanya kazi kwa bidii na uaminifu ili kuendelea kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya afya nchini.
Trending
- Hii ndiyo Shule ya Sekondari Mbeya DAY!! inazidi kung’ara
- Viziwi waipongeza Serikali huduma za Afya, waomba alama itakayowatambulisha katika usafiri
- KAILIMA: WENGI WAJITOKEZA KUBORESHA AU KUJIANDIKISHA KATIKA DAFTARIO LA KUDUMU LA WAPIGA KURA
- Bodi ya TASAC yaridhishwa utekelezaji wa maagizo kwa TPA
- TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM (2020-2025) MBUNGE VITI MAALUM MKOA WA MBEYA – MH. MAHUNDI
- Tulia Traditional Dances Festival 2024 Kurundima Mkoani Mbeya
- Uvumi kifo cha Muimbaji wa Injili Bonny Mwaitege Wazazi Waiomba Serikali kuchukua hatua
- Mtoto adaiwa kumuua baba yake mzazi kwa shambulio la mwili