Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya imepokea vifaa tiba vya kisasa monitor 15 kwa lengo la kuboresha huduma za uangalizi kwa watoto wachanga. Vifaa hivi, vilivyotolewa na Madau wa Maendeleo GOAL 3, vinatarajiwa kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za afya kwa watoto wanaohitaji msaada wa haraka na wa kitaalamu.
Akikabidhi vifaa tiba hivyo Mwamvuwa Mika Meneja Mradi Tanzania amesema thamira ya Goal 3 ni hakikisha Watoto wachanga wananzaliwa katika mazingira mazuri na pia wanapata huduma ambayo ni bora.
“Kwa kipindi hiki tumefika hapa hospitali ya rufaa ya kanda Mbeya kwaajili ya kufunga Impala monitors kwenye kitengo cha NIKU ili kuweza kuwasaidia Watoto wachanga wanaozaliwa kabla ya muda. Ningependa pia kutoa shukrani zangu za dhati kwa Uongozi wa hospitali kwasababu tumeweza kushirikiana hadi kwa hatua hii tuliofika leo ambapo tumeshazifunga monitors 15 na zimeshaanza kutoa huduma kwa Watoto walio wodini na pia tutaendelea kushirikiana ili kuwafika Watoto wengine walio kwenye hospitali zingine ” – Mwamvuwa
Akizungumza mara baada ya kupokea vifaa hivyo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya Bi. Myriam Msalale amemshukuru Madau wa maendeleo GOAL 3 kwa kuichagua Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kufanya kazi nayo na kuvipatia vifaa tiba hivyo ambavyo vimekuja kwa wakati na vitatusaidia sana katika kuboresha huduma kwa watoto wachanga na kutoa wito kwa watumiaji wa vifaa tiba hivyo kuvitunza kwa uangalifu wa hali ya juu ili viweze kudumu kwa muda mrefu na kuwahudumia Watoto waliokuja kupata matibabu.
.
Nae Dkt.Rehema Marando Daktari Bingwa mbobezi wa watoto wachanga, amesema kuwa msaada huo umeleta manufaa makubwa kwa watoa huduma na Watoto ambapo vitawezesha kuboresha huduma na kuongeza ufanisi wa utoaji wa matibabu na uangalizi wa hali ya juu kwa Watoto wachanga.