Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Maafisa wa Shirika la Umeme [TANESCO] Tawi la Mbeya linamshikilia Ikupa Mwakibibi [32] mjasilimali na mkazi wa Sae Jijini Mbeya kwa tuhuma za kuhujumu miundombinu ya Shirika la Umeme kwa kujiunganishia umeme kinyume na utaratibu wa shirika hilo.
Mtuhumiwa alikamatwa Agosti 18, 2025 saa 9:30 alasiri Mtaa wa Sae uliopo Kata ya Ilomba Jijini Mbeya katika oparesheni za pamoja za Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Shirika la Umeme [TANESCO] ambapo baada ya kupekuliwa katika nyumba yake mtuhumiwa alikutwa akiwa na mita za umeme 19, rimoti za TANESCO 45 pamoja na waya rola 25 vyote vikiwa ni mali ya shirika la TANESCO.