Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na uchunguzi wa tukio la
mauaji ya aliyekuwa Mwanachuo wa mwaka wa kwanza katika Chuo
Kikuu cha Mzumbe ndaki ya Mbeya kitivo cha sheria aitwaye Shairose
Michael Mabula [21].
Awali mnamo tarehe 14 Septemba, 2025 Baba mzazi wa marehemu
aitwaye Dkt Michael Mabula alifika kituo kikuu cha Polisi Mbeya na kutoa
taarifa ya kupotea kwa binti yake aitwaye Shairose Mabula ambapo
jalada la uchunguzi lilifunguliwa na kuanza ufuatiliaji ili kumpata. mnamo
tarehe 16 Septemba, 2025 saa 5:00 usiku huko Mtaa wa Morovian uliopo
Kata ya Isyesye Jijini Mbeya ilipokelewa taarifa ya ajali ya moto ambapo
Askari walifika eneo la tukio na kukuta kibanda kinateketea kwa moto.
Baada ya uchunguzi ilibainika kuna mwili wa mtu mmoja jinsia ya kike
unaugua ambaye kwa wakati huo hakuweza kutambulika.
Mwili wa marehemu ulichukuliwa na kuhifadhiwa Hospitali ya Rufaa
Kanda Mbeya na baada ya uchunguzi wa kitabibu na kuhusisha ndugu
ilibainika kuwa mwili huo ni wa Shairose Mabula aliyekuwa anatafutwa
baada ya kuripotiwa kupotea.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na uchunguzi wa kina
ikiwemo uchunguzi wa kisayansi ili kubaini na kutambua mwili wa
marehemu na kuwakamata waliohusika na mauaji haya. Aidha, Jeshi la
Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa yeyote mwenye taarifa
zitakazofanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa azitoe. Pia, Jeshi la Polisi
Mkoa wa Mbeya linaendelea kutoa rai kwa jamii kuacha tabia ya
kujichukulia sheria mkononi na kusababisha madhara makubwa kama
mauaji.
Imetolewa na:
Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa Mbeya.
Trending
- Mwanachuo Mzumbe Afariki Kikatili Mbeya ni Binti wa Dkt. Michael Mabula
- Dourmohamed Issa: Mwalunenge na Samia Wapewe Kura za Kutosha
- Mwalunenge: Asimama na Wanyonge, Atangaza Mpango wa Elimu kwa Watoto Wasiojiweza
- Nilipoteza Mali Yote Baada ya Talaka, Lakini Hatua Niliyopiga Ilinirudishia Kila Kitu
- BENKI YA NMB YATAHADHARISHA WALIMU UTAPELI MATUMIZI YA ATM CARD
- Nilishindwa Mitihani Mara Nne, Lakini Hatua Niliyopiga Ilinifanya Nifaulu Kwa Alama za Juu
- PASTOR EZEKIEL ODERO AWAOMBA WATANZANIA KUDUMISHA AMANI KUELEKEA UCHAGUZ! MKUU
- Nilikataliwa na Wanaume Wote Lakini Hatua Niliyopiga Ilinifanya Niolewe na Tajiri