Jiji lote lilijua kesi yangu ya talaka. Ilikuwa gumzo mitaani na hata kazini. Siku ya hukumu nilihisi dunia imenipotea. Nilipoteza nyumba yangu, magari, na hata biashara yangu ikagawanywa kwa mume wangu wa zamani. Nilipokea makaratasi ya hukumu nikiwa nimekaa kimya, machozi yakinibubujika, nikijiuliza nitaanzia wapi tena. Majirani waliniangalia kwa huruma, wengine wakinong’ona kwamba maisha yangu yalikuwa yamefika mwisho.
Mali niliyojenga kwa miaka mingi ya jasho ilipotea kwa dakika chache tu za kusoma hukumu. Nililazimika kuondoka kwenye nyumba niliyoinunua kwa mikopo na kwenda kukaa na shangazi yangu kwa muda. Nilikuwa nimevunjika moyo na kila nilichokiona kilinikumbusha maisha yangu ya ndoa. Nilipoteza hamu ya kula, nilianza kupoteza uzito, na hata kuzungumza na watu nikawa sina nguvu.
Kesi ya rufaa niliyojaribu kufungua haikusaidia chochote kwa sababu upande wa mume wangu ulikuwa na nguvu na wakili wao alikuwa na ujuzi mkubwa.
Nilianza kuamini kwamba huu ndio ulikuwa mwisho wangu. Marafiki walinambia nianze upya maisha, lakini nilijua haki yangu ilikuwa haijapatikana. Nilikuwa na ushahidi kwamba nilichochangia katika kujenga mali ile kilikuwa kikubwa kuliko chake, lakini mahakama haikuzingatia. Soma zaidi hapa