Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza kuwa Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utafanyika Jumatano, Oktoba 29, 2025.
โ
Vituo vya kupigia kura vitafunguliwa saa 1:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni.
โ
Vituo vya magereza vitafunguliwa saa 2:00 asubuhi hadi saa 9:00 alasiri.
โ
Kila mpiga kura anatakiwa kufika kituoni na kadi yake ya kupigia kura.
โ
Waliopoteza kadi wataruhusiwa kutumia NIDA, leseni au pasi ya kusafiria endapo jina lipo kwenye daftari la wapiga kura.
๐๏ธ Taarifa hii imetolewa na Ms. Anamary Joseph Mbunga, Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Mbeya Mjini โ tarehe 19 Oktoba 2025.

