Sikuwahi kufikiria kuwa mtu niliyempenda kwa moyo wangu wote angeweza kuniacha bila hata neno. Tulikuwa tumepanga maisha yetu, tukawa tumenunua vitu vya nyumba, tukapanga ndoto za watoto na biashara. Lakini siku moja asubuhi, aliniambia kwa sauti tulivu, “Nahisi nimechoka, sitaki tena.”
Nilidhani anatania. Nilijaribu kuuliza sababu, lakini hakusema. Aliondoka bila hata kuangalia nyuma. Nilijikuta nikipoteza kila kitu furaha, hamasa, hata usingizi. Nilikuwa kama kivuli cha mimi niliyemjua.
Miezi ya kwanza ilikuwa kama kuzimu. Nililia usiku kucha, nikikumbuka maneno yake na tabasamu lililokuwa limejaa ahadi tupu. Watu walinicheka, wengine wakasema nimeachwa kwa sababu ya mikosi. Nilihisi aibu hata kutoka nyumbani.
Nilijaribu kujisahaulisha kwa kazi, lakini bado nilihisi upweke mkubwa. Wakati mwingine nilijikuta nikimuandikia ujumbe usiopelekwa, nikifuta machozi yangu kimya kimya. Nilijua lazima nifanye kitu ili nijinasue katika mateso hayo. Soma zaidi hapa

