Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene amewashukuru watanzania kwa kuonyesha utulivu na uzalendo katika kuilinda amani ya Tanzania na kudumisha utulivu wakati nchi ikienda kuazimisha miaka 64 ya Uhuru wa Tanzania Bara…..
Ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa ukaguzi wa hali ya ulinzi na usalama katika mitaa mbalimbali ya jijini Dar es Salaam huku Vyombo vya Ulinzi na usalama vikiendelea kuimarisha ulinzi katika maeneo tofauti nchini ambapo wananchi nao wametoa maoni yao.

