*DKT. MWIGULU AMBANA MKANDARASI UJENZI WA BARABARA YA KITAI-RUANDA*
_Aaagiza kukamatwa kwa hati yake ya kusafiria hadi atakapokamilisha ujenzi_
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kumsimamia vema mkandarasi anayejenga barabara ya Kitai hadi Ruanda ili aweze kuendana na kasi iliyotarajiwa.
Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema tayari Serikali ilikwishalipa fedha za ujenzi wa barabara hiyo kwa kutambua umuhimu wake kwenye uchumi wa mkoa huo na Taifa kwa ujumla.
📍Songea-Tanzania
🗓️Desemba 16, 2025

