Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na Aga Khan Health Service Tanzania zimeingia katika makubaliano ya ushirikiano wa kimkakati unaolenga kuboresha utoaji wa huduma za afya kwa Watanzania. Akizungumza jijini Mbeya, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, Dkt. Godlove Mbwanji, alisema ushirikiano huo utawezesha kubadilishana ujuzi na uzoefu kati ya sekta ya umma na binafsi kwa manufaa ya wananchi.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Aga Khan Health Service Tanzania, Sisawo Konteh, alisema makubaliano hayo yataimarisha huduma za kliniki, kujenga uwezo wa watumishi, kuboresha mifumo ya ubora na kusaidia hospitali hiyo kupata ithibati. Ushirikiano huo pia utahusisha mafunzo, tafiti na kuendeleza huduma bingwa ikiwemo saratani na magonjwa ya moyo, pamoja na kukuza utalii wa tiba katika mkoa wa Mbeya.
Trending
- Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na Aga Khan Zaanzisha Ushirikiano wa Kuboresha Huduma za Afya
- Shule ya Sekondari Utengule Usangu, H
- Mradi wa Barabara Mlima Nyoka Wamfikisha MCC ASAS, Ataka Kero za Wananchi Zitokomee
- Mradi wa Soko la Matola Wakwama, Meya na MNEC Wakanusha Kukamilika Mei
- JK KWA MFALME MSWATI III KUJADILI UPATIKANAJI WA FEDHA ZA MIRADI YA AFYA KWA NCHI WANACHAMA WA ECSA
- Halmashauri Yaipongeza Mbeya UWSA Kwa Mradi wa Maji, Asema Utakuza Uwekezaji
- Mpango wa Maendeleo 2026/27: Kasaka Apongeza Mafanikio, Aomba Maboresho
- Msafara Wasimama Soweto, Mbunge Mwalunenge Aamuru TANROADS Kuondoa Dimbwi la Miaka 3 Mara Moja

