Mkurugenzi Mtendaji wa Equity For Tanzania Limited- EFTA Bwana Nicomed Bohay akizungumza na wageni waalikwa wakati wa uzindunzi wa Hati Fungani za EFTA tukio lilofanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam katika Hotel ya Kilimanjaro Hyatt Regency.
Wageni mbalimbali, wakiwemo wadau wa sekta ya fedha, wawekezaji na wawakilishi wa taasisi za kifedha, wakifuatilia kwa makini tukio la uzinduzi wa EFTA Corporate Bond ya Shilingi bilioni 50, lililofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. Uzinduzi huo uliashiria hatua mpya ya kuimarisha upatikanaji wa mtaji wa muda mrefu kwa sekta za uzalishaji nchini.
Wajumbe wa jopo la majadiliano wakichangia mada wakati wa uzinduzi wa EFTA Corporate Bond ya Shilingi bilioni 50 jijini Dar es Salaam, wakijadili umuhimu wa mtaji wa muda mrefu katika kuimarisha sekta za uzalishaji na kukuza masoko ya mitaji nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa EFTA, Nicomed Bohay, akichangia mjadala wa jopo wakati wa uzinduzi wa Hati Fungani ya Sh bilioni 50 jijini Dar es Salaam, akieleza namna mpango huo unavyolenga kuimarisha mtaji wa muda mrefu kwa sekta za uzalishaji na kutoa fursa ya uwekezaji kwa umma.



Wageni mbalimbali, wakiwemo wadau wa sekta ya fedha, wawekezaji na wawakilishi wa taasisi za kifedha, wakifuatilia kwa makini tukio la uzinduzi wa EFTA Corporate Bond ya Shilingi bilioni 50, lililofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. Uzinduzi huo uliashiria hatua mpya ya kuimarisha upatikanaji wa mtaji wa muda mrefu kwa sekta za uzalishaji nchini.

Muhumiza Buberwa, Meneja wa Kanda ya Dar es Salaam wa Benki ya CRDB, akizungumza wakati wa uzinduzi wa EFTA Corporate Bond jijini Dar es Salaam, akieleza umuhimu wa ushirikiano kati ya benki na masoko ya mitaji katika kuimarisha ufadhili wa sekta za uzalishaji nchini.
Meneja wa Maendeleo ya Soko kutoka Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), David Magabe, akizungumza wakati wa uzinduzi wa EFTA Corporate Bond jijini Dar es Salaam, akisisitiza umuhimu wa masoko ya mitaji katika kuhamasisha mtaji wa muda mrefu kwa sekta za uzalishaji nchini.

Mkuu wa Idara ya Rasilimali Watu na Sheria wa Equity for Tanzania Limited (EFTA), Lucy Bwana, akifuatilia kwa makini uzinduzi wa EFTA Corporate Bond ya Shilingi bilioni 50 uliofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency, Dar es Salaam, tukio lililolenga kuimarisha upatikanaji wa mtaji wa muda mrefu kwa sekta za uzalishaji nchini.



.jpeg)
Wafanyakazi wa Equity for Tanzania Limited (EFTA) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi rasmi wa EFTA Corporate Bond ya Shilingi bilioni 50 jijini Dar es Salaam, wakionesha mshikamano na dhamira ya kuimarisha ufadhili wa muda mrefu kwa sekta za uzalishaji nchini.
EFTA YACHOCHEA UCHUMI KWA HATI FUNGANI YA BILIONI 50



