Author: Mbeya Yetu

Leo 1 Oktoba 2025 Mgombea Ubunge wa Jimbo la Uyole kwa tiketi ya CCM Dkt Tulia Ackson amesema ahadi zinazotolewa na Chama cha Mapinduzi kwa Wananchi ni zauhakika kwani zimekuwa zikitekelezeka kwa uhakika kutokana na Msimamizi Mzuri unaofanyika Chini ya Serikali inayoundwa na Chama hicho. Akizungumza na Wananchi Kwenye Mkutano wake wa Kampeni eneo la Makondeko Sokoni Dkt. Tulia amesema mifano ya Jambo hilo ipo wazi, wakati anaomba ridhaa ya kuliongoza Jimbo la Mbeya Mjini aliahidi kupatikana kwa hospital ya Wilaya Jambo ambalo limekamika kwa kupata hospitali ya Igawilo ambayo inavifaa na Wataalamu wa kutosha, pia CCM iliahidi Ujenzi wa…

Read More

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Tulia Ackson amesema kwenye Sekta ya kilimo ndani ya Kata ya Iganjo Mgombea Uraisi kwa tiketi ya CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya Kazi Kubwa hasa Kuhakikisha Mbolea za Ruzuku na Pembejeo zote za kilimo hivyo ataendelea kuongeza upatikanaji maradufu wa Ruzuku na Pembejeo za kilimo. Dkt. Tulia amesema anafahamu kwamba ndani ya kata hiyo Kuna kilimo cha umwagiliaji hivyo atahakikisha skimu zote za umwagiliaji zinabireshwa zadisi ili wakulima Wafanye kilimo Bora hivyo ifikapo 29 Oktoba 2025 Wananchi wakapige Kura nyingi kwa CCM ili wakulima wa Jimbo la…

Read More

Zaidi ya wanaume 1000 kutoka katika mji wa Tunduma mkoani Songwe wamefunga Barabara kwa saa kadhaa wakifanya matembezi ya aina yake na kuwaacha watu midomo wazi barabarani wakiadhimisha mwaka mmoja wa muungano wa kikundi chao maalum Cha kijamii chenye lengo la kuinuana na kusaidiana wao kwa wao.

Mwenyekiti wa kikundi hicho Herode Jivava anasema waliamua kuanzia kikundi hicho ili kumkomboa mwanaume na aibu ambazo amekuwa akikumbana nazo pindi linapotokea jambo la furaha ama huzuni hivyo wao wapo kwaajili ya kumuinua na kumrejeshea heshima mwanaume huyo.

Read More

Mbeya, Septemba 28, 2025 – Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limefanikisha operesheni maalum iliyopelekea kuuawa kwa watuhumiwa waliodaiwa kuhusika na utekaji na mauaji ya kikatili ya Shyrose Michael Mabula [21], mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu cha Mzumbe Ndaki ya Mbeya, Kitivo cha Sheria.

Shyrose aliripotiwa kutekwa nyara Septemba 14, 2025 na mwili wake kupatikana Septemba 16 usiku katika Mtaa wa Morovian, Kata ya Isyesye Jijini Mbeya ukiwa umechomwa moto. Uchunguzi uliofanywa na Polisi uliwakamata watuhumiwa watatu: Marwa Nyahega John [25], Edward Christopher Kayuni, na Websta William Mwantebele [27], ambao walikiri kupanga njama za kumteka kwa lengo la kujipatia fedha kutoka kwa baba yake, Dkt. Mabula Michael.

Kwa mujibu wa Polisi, baada ya kushindikana kwa mpango huo, walimnywesha sumu ya kuulia magugu aina ya Round Up bila mafanikio, kisha wakamnynonga kwa kamba na kuuchoma moto mwili wake.

Mnamo Septemba 27, 2025, wakati wa operesheni katika Kijiji cha Chalangwa, wilayani Chunya, watuhumiwa Edward na Websta walijaribu kukimbia na kuwashambulia askari kwa kisu. Polisi walifyatua risasi za tahadhari, lakini walipokaidi amri, walijeruhiwa kwa risasi na kufariki dunia wakipelekwa hospitalini. Mtuhumiwa wa tatu, Marwa, naye alifariki baada ya kujirusha kutoka kwenye gari la Polisi wakati akipelekwa kuonyesha vielelezo.

Katika upekuzi, Polisi walipata pingu mbili, vitambulisho feki vya JWTZ, simu zenye picha za utekaji na mawasiliano yao, pamoja na taarifa kwamba kidole na nguo za marehemu vilikuwa vimepelekwa kwa mganga wa jadi kwa ajili ya zindiko. Mganga huyo kwa sasa anatafutwa.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeonya vijana na wananchi kwa ujumla kuacha tamaa ya mali kwa njia za haramu, na kusisitiza kuwa uhalifu haulipi na mkono wa sheria utawafikia popote pale.

Imetolewa na:
Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Mbeya

Read More