Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- Vigeregere na Shangwe! Dkt. Tulia Aongoza Mapokezi ya Mabomba ya Mradi wa Maji kutoka Mto Kiwira
- Nsomba Ampongeza Dk. Tulia Ackson kwa kutoa huduma ya matibabu ya Macho Bure Jijini Mbeya
- Dkt. Tulia Ackson Aongoza Zoezi la Upimaji na Matibabu ya Macho Bure Jijini Mbeya
- JK AWAILISHA SALAMU ZA RAIS SAMIA KWA KEPTENI IBRAHIM TRAORE, KIONGOZI WA KIJESHI WA BURKINA FASO MJINI OUAGADOUGOU LEO
- WANANCHI WAIBUA TAHARUKI OFISI ZA VITAMBULISHO VYA NIDA MBEYA AFISA MSAJILI MBEYA ATOA UFAFAUZI
- Wakazi wa Mwansekwa na Igodima Wapongeza Upatikanaji wa Maji Safi
- Mbunge Masache: “Rais Samia ameboresha huduma za Afya na Elimu;Mitano tena kwake!!”
- “Wakulima Festival 2025: Tamasha Kubwa la Kilimo Kufanyika Mbeya kwa Ushirikiano wa Taasisi 100
Browsing: Video Mpya
#mbeyayetutv
Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 24 Mei 2024, ametembelea Kanisa la Mtakatifu Bikira Maria lililopo Cairo nchini Misri, eneo ambalo Bikira Maria alijificha na Mtoto Yesu kufuatia tishio la Mfalme Herode kutaka kumuua Mtoto Yesu. Ziara hii inasisitiza umuhimu wa kuenzi, kudumisha na kuendeleza amani, umoja na kuwa na uelewa wa pamoja katika imani na utamaduni wetu.
Mashauri matatu yalizofunguliwa Mahakama ya Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya kwa Hati ya dharula na Aidan Msigwa dhidi ya Lucas Mbwiga Mwapenza kuhusiana na mgogoro wa Kitalu cha uchimbaji madini ya dhahabu eneo la Kisumain Kijiji cha Ifumbo Kata ya Ifumbo Wilaya ya Chunya yamepokelewa na Hakimu James Mhanusi kwa ajili ya kusikilizwa.
Hati hiyo imewasilishwa Mahakama ya Wilaya na Wakili wa kujitegemea Jacqueline Massawe kwa niaba ya Aidan Msigwa wakati Lucas Mwampenza akitetewa na Wakili Boniphace Mwabukusi akisaidiwa na Wakili Irene Mwakyusa.
Mashauri yaliyowasilishwa Mahakamani na Wakili Jacqueline Massawe kwa niaba ya Aidan Msigwa ni pamoja na kesi ya msingi ya kutaka kulimiliki eneo lake analodai kulimiliki kihalali baada ya kulinunua,shauri la pili ni kusudio la zuio la kutofanyika kwa shughuli zozote katika eneo hilo na shauri la tatu ni kuendelea na shughuli licha ya kuwepo kwa zuio la Mahakama.
Wakili Massawe amempatia Wakili Mwabukusi Hati ya dharula na nakala kuwasilishwa Mahakamani na Wakili Mwabukusi naye kuwasilisha pingamizi mbele ya Mahakama.
Baada ya kupokea nyaraka za pande zote mbili Hakimu James Mhanusi ameahirisha shauri hilo hadi mei 13,2024 Mahakama itakapoanza kuzisikiliza pande zote mbili.
Nje ya Mahakama Wakili Mwabukusi ameeleza mashauri anayodaiwa katika Mahakama hiyo kupitia Hati ya dharura kuwa ni pamoja na kesi ya msingi ya kutaka kulimiliki eneo lake analodai kulimiliki kihalali baada ya kulinunua,shauri la pili ni kusudio la zuio la kutofanyika kwa shughuli zozote katika eneo hilo na shauri la tatu ni kuendelea na shughuli licha ya kuwepo kwa zuio la Mahakama.
Mahakama pekee ndiyo inatarajiwa kuumaliza mgogoro huo ili kuleta amani katika Kata ya Ifumbo.
Mgogoro umeibuka baina ya Lucas Mbwiga na Aidan Msigwa Wawekezaji wawili wa machimbo ya dhahabu katika Kijiji cha Ifumbo Kata ya Ifumbo Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya ambapo kila mmoja anadai kulimiliki kihalali eneo la Kisumain lililokuwa na leseni ya uchimbaji wa madini kwa jina la Daud Mwantavila ambalo linadaiwa kupangishwa kwa Lucas bila ridhaa ya familia huku Aidan Msigwa akidai kulinunua kisheria na kubadilisha umiliki wa leseni kutoka kwa Daud na kuja kwake tangu April 22,2024.
#mbeyayetutv
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Cde Juma Z. Homera amefika Mlima Kawetele uliopolomoka Alfajiri ya Leo na Kusababisha Kufukiwa kwa Nyumba 20, Ng’ombe Wanne na Kuharibika kwa Miundombinu ya Shule ya Generation katika Mtaa wa Gombe Kata ya Itezi Halmashauri ya Jiji la Mbeya.
Akizungumza baada Kuwasili eneo la Tukio RC Homera amekanusha Uvumi unaozagaa Mtandaoni ukidai Kuna Maafa katika tukio hilo ambapo amesema zaidi ya hivyo vilivyotajwa Aya ya Kwanza hakuna Madhara mengine Wala Maafa kama inavyoripotiwa na Baadhi ya Watu.
Aidha Homera ameiagiza Halmashauri ya Jiji la Mbeya kufanya Tathimini juu ya Waathirika hasa wale wasio na Malazi ya Kulala wahakikishe wanapatiwa Sehemu hizo wakati huu ambao Serikali inaendelea kupambana kuhakikisha Hali inakuwa Sawa katika Maeneo hayo.
Pia amekiagiza Kitengo Cha Ardhi Halmashauri ya Jiji la Mbeya kuacha kuwapimia Wananchi Viwanja eneo lenye Changamoto hasa ya Mkondo wa Maji kwa kufanya Kwao hivyo kutasababisha Matatizo kama hayo ambayo yangeweza kuzuilika.
Tukio hilo limetokea Alfajiri ya Kuamkia Leo ambapo chanzo Chake ni Mvua zinazoendelea Kunyesha Mfululizo na Matukio yanayofanana na haya yamekuwa yakitukia Mikoa Mbalimbali ikiwemo Mikoa ya Arusha na Lindi.
Watu wawili jinsi ya kike wakazi wa Kiwanja Kata ya Mbugani Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya wanadaiwa kuuawa na mtoto mwingine mwenye umri wa miaka sita kujeruhiwa kwa vitu vyenye ncha kali nyumbani kwao.
Uchunguzi wa awali umebaini kuwa aliyeuawa ni mwalimu Herieth Lupembe wa shule ya msingi Mbugani na mwingine ni Ivon Tatizo Haonga(16) mwanafunzi wa kidato cha kwanza sekondari ya lsenyela aliyekuwa anaishi naye.
Taarifa za mauaji hayo zilipatikana jioni machi 30,2024 baada ya mwalimu huyo kutofungua duka lake na simu yake kutopatikana pia kutoonekana kanisani wakati si kawaida yake.
Baadhi ya mashuda wamedai kuwa aliagiza bidhaa za dukani kutoka Mbeya baada ya kutoonekana bidhaa hizo ziliachwa nje ya duka lake lililopo mita hamsini kutoka nyumbani kwake.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Edith Swebe Machi 30,2024 ameshiriki katika kongamano la Pasaka la Ushirika wa Kikristo wa Wanafunzi Tanzania (UKWATA) wa Shule za Sekondari Mkoa wa Simiyu ambalo limefanyika katika shule ya Sekondari Itilima iliyopo Wilaya ya Itilima.
Kamanda Swebe alipata fursa ya kuongea na vijana hao wa UKWATA Mkoa wa Simiyu na kuwahasa kujiepusha na matumizi mabaya ya Mitandao ya kijamii kwa kuangalia picha zisizo na maadili kitendo ambacho kinaweza kusababishia madhara ya afya ya akili na badala yake watumie mitandao ya kijamii kwa lengo la kujifunza.