Browsing: Video Mpya

Taasisi ya Tulia Trust inayoongozwa na Rais wa Mabunge Duniani Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt Tulia Ackson imetoa msaada wa vyombo vya kuhubiria Msikiti wa Masjid Bi Fatma Nzovwe Jijini Mbeya.
Akikabidhi vifaa hivyo kwa niaba ya Dkt Tulia Ackson Afisa Habari wa Taasisi hiyo Joshua Mwakanolo amesema lengo ni kutekeleza ombi la Msikiti huo kwa Mbunge ambapo waliomba vipaza sauti kwa ajili ya ibada.

Kwa niaba ya Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Mbeya msemaji wake Shekhe Ibrahim Bombo mbali ya kushukuru amewaomba waumini kumuombea dua ya heri huku akitaka vyombo hivyo vitunzwe kwa uangalifu.

Naye Hemed Kipengele kwa niaba ya Waumini ametoa neno la shukurani akimshukuru Mbunge kwa kutoa vifaa hivyo bila kujali itikadi za Kidini.

Aidha Justin Kayuni Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Ndanyela ameipongeza Taasisi ya Tulia Trust kwa kutoa vifaa hivyo kwani vitasaidia kueneza neno la Mungu.

Hatimaye Abdalah Yundu Shekhe Mkuu wa Wilaya ya Mbeya ameongoza dua ya kumuombea Dkt Tulia Ackson katika kazi zake za kila siku.

Dkt Tulia amekuwa akitoa misaada mbalimbali bila kujali itikadi za Kidini na Kisiasa ambapo hivi karibuni amefanikisha ujenzi wa Misikiti ya Tukuyu Mjini,Kiwira Wilayani Rungwe na Uyole Jijini Mbeya.

Zaidi ya bilioni kumi na Moja zimetumika kukamilisha ujenzi wa miradi mbalimbali katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya ndani ya miaka mitatu tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassani kuapishwa kuwa Rais wa awamu ya sita kutokana na aliekuwa rais wa awamu ya Tano kufariki Dunia mwanzoni mwa mwaka 2022 Hayati Dkt.Pombe Joseph Magufuri.

Hayo yamebainishwa na Mganga mfawidhi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya Dkt.Abdallah Mmbaga wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari juu ya hali ilivyo tangu Dkt.Samia Suluhu Hassan kuwepo madarakani.

Baadhi ya wananchi waliopo Mkoani Mbeya wamezungumzia hali ya huduma ilivyo katika hospitali hiyo wakisema maboresho makubwa yaliyofanywa na serikali yamefanya hospitali hiyo kuwa kimbilio la haraka kwao huku wakiwapongeza watumishi wa hospitali hiyo kuwa na lugha nzuri kwa wagonjwa tofauti na zamani.

Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Mbeya huhudumia wakazi wa Wilaya za Mbeya,Kyela,Chunya,Mbarali na Rungwe.

Jeshi la Polisi Nchini limesema Machi 20, 2024 lilitoa taarifa kuhusiana na kifo cha Omary Saimon Msamo kilichotokea huko Wilayani Karatu Mkoa wa Arusha Machi 16, 2024.

Akitoa taarifa hiyo leo machi 26,2024 Msemaji wa Jeshi la Polisi Nchini Naibu Kamishna wa Polisi DCP David Misime amesema Jeshi hilo lilieleza mazingira ya tukio hilo ambapo amebainisha kuwa ilibidi kushirikisha wataalam mbalimbali wakiwepo wachunguzi wa matukio ya vifo.

DCP Misime aliendelea kueleza kuwa Timu ya uchunguzi wa tukio hilo ilipofanya uchunguzi wa tukio hilo ilibaini kuwa kifo chake hakikuwa cha kawaida bali ilikuwa ni Mauaji.

Aidha Msemaji wa Jeshi hilo alisema Baada ya kubaini hivyo Jeshi hilo lilianza uchunguzi wa mauaji hayo ambapo lilibaini waliohusika wa mauaji hayo.

Sambamba na hilo amebainisha kuwa uchunguzi umebaini kuwa malengo yalikuwa ni kumpora Omary Saimon Masamo chochote kile watakacho mkuta nacho.

Misime ameviambia vyombo vya habari kuwa Waliohusika na mauaji hayo tayari wamekamatwa na wamekutwa wakiwa na simu ya marehemu huku fedha walizompora kiasi cha Shilingi 200,000/= wakiwa tayari wameshagawana na kuzitumia.

Waliokamatwa ni Anthony Paskali ambaye anajulikana kwa jina maarufu Lulu na Emmanuel Godwin Jeseph anayejulikana kwa jina maarufu la Emma wote wakiwa ni wakazi wa Wilaya ya Karatu.

Taratibu zilizobaki za kiuchunguzi zinakamilishwa ili hatua nyingine za kisheria ziweze kufuata.

Pia DCP Misime amesema Jeshi la Polisi linaendelea kutoa tahadhari kwa baadhi ya watu kuacha kueneza taarifa za uwongo, chuki na uzushi dhidi ya mtu mwingine au taasisi kwa ajili ya malengo yao binafsi kwani kwakufanya hivyo watakuwa wanaukaribisha mkono wa sheria uweze kuwafikia na kuchukuliwa hatua.

#mbeyayetutv
Mkuu wa mkoa wa Mbeya Juma Homera amevunja ukimya na kuweka mambo hadharani kwa kuelezea hisia zake juu ya kile kinachoelezwa na baadhi ya wanasiasa wilayani’Namtumbo mkoani Ruvuma.
Akiwa katika iftari maalumu iliyoandaliwa na Taasisi ya Site Trust Foudation na Site Fm zinazosimamiwa na wake zake Imani na Jasmin.
‘’Namtumbo ni Nyumbani kwetu Nimezaliwa Namtumbo sijaja kufanya siasa tuwaunge mkono viongozi wetu’’amesema Homera

WANANCHI MBEYA WALIA KUVAMIWA NA TAZARA

Wakazi wa Iyunga,Ivumwe,ltuha,ltezi na Nsalaga Jijini Mbeya wameiomba Serikali kutolea ufafanuzi mgogoro wa ardhi baina yao na Shirika la Reli Tanzania na Zambia(TAZARA)baada ya Shirika hilo kuweka mawe(Bicons)katika maeneo yao sanjari na kuwataka wabomoe nyumba zao zinazodaiwa kuwepo mita hamsini ndani ya hifadhi ya reli kinyume na makubaliano.

Wananchi hao kwa nyakati tofauti wakiwa na nyaraka mbalimbali kuhusiana na mgogoro huo wamepaza sauti zao baada ya kugonga ukuta ofisi zote ikiwemo TAZARA na ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbeya.

Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Timotheo Mnzava leo Machi 14, 2024, imetembelea miradi inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufungua utalii wa Malikale kwenye magofu ya Kisiwa cha Kilwa Kisiwani ikiwa ni juhudi mpya za kuongeza zao jipya la utalii huo.

“Tunaposema tunapongeza juhudi za Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kwa vitendo kama hivi. Hapa katika miaka hii mitatu Serikali yake imetoa fedha kuendeleza utalii wa malikale ikiwemo boti mpya ya kisasa ambayo watalii wanaweza kuona ndani ya maji, gati la kushuka abiria, jengo jipya la kufikia abiria na miundombinu mingine ambayo imechagiza idadi ya watalii kuongezeka hapa kutoka wastani wa 2900 hivi hadi 6,400. Haya ndio mafanikio yenye maono,” alisema Mhe. Mnzava.

Ziara hiyo pia walikuwepo Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki, Naibu wake, Mhe. Dunstan Kitandula, Katibu Mkuu Dkt. Hassan Abbasi na watendaji waandamizi kutoka Idara za Wanyamapori, Malikale na Misitu.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Ombeni Manase Kilawa [43] mkazi wa
Lusese Wilaya ya Mbarali anayetuhumiwa kumuua mke wake aitwaye Happynes
Gervas Mwinuka [40] mkazi wa Kijiji cha Lusese kwa kumkata na kitu chenye ncha kali.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia Machi 13, 2024 Kitongoji cha Masista, Kijiji cha
Lusese, Wilaya ya Mbarali baada ya kutokea ugomvi baina ya wana ndoa hao wakiwa
nyumbani kwao na kupelekea mtuhumiwa Ombeni Kilawa kuchukua kisu na kumkata
mke wake shingoni.
Uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi baada
ya mtuhumiwa kumhisi na kumtuhumu mke wake kuwa na mahusiano ya kimapenzi na
wanaume wengine.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, linatoa wito kwa jamii kuwa pindi wanapopatwa na
tatizo au changamoto katika ndoa zao isiwe suluhisho lake kujichukulia sheria mkononi
bali ni kutafuta ushauri kwa wazazi, walezi, wasimamizi wa ndoa, viongozi wa dini,
katika madawati ya jinsia na watoto waliopo kila Wilaya ya Kipolisi, katika ofisi za
halmashauri au kutafuta haki kwenye Mahakama ili kuepuka madhara.

MWALUNENGE AKAGUA MAENDELEO YA UKARABATI UWANJA WA SOKOINE NA KUAHIDI MAKUBWA

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)Mkoa wa Mbeya Patrick Mwalunenge amekagua maendeleo ya ukarabati wa uwanja wa Sokoine kutekeleza agizo la TFF la kuufanyia ukarabati uwanja huo eneo la uwanja na uzio.

Hata hivyo Mwalunenge amebainisha ukarabati mkubwa utafanyika wa kuezeka paa na ufungaji wa taa ili uwanja huo uweze kutumika kwa michezo ya kimataifa hata nyakati za usiku.