Browsing: Video Mpya

Ikiwa ni msimu wa tano tangu kuanzishwa kwa Tulia Trust Uyole Cup leo Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mh. Beno Malisa amezindua rasmi msimu wa Tano wa 2025 akiwataka wananchi kutofanya vurugu ili washuhudie vipaji kutoka Jiji la mbeya. Kwa upande wake Jaqline Boazi meneja wa Tulia Truss ameeleza namna wananchi wanavyonufahika na timu 35 kushiriki huku kaimu mwenyekiti wa wa chama cha mpira mkoa wa Mbeya akieleza namna matarajio yao ya kupata vipaji mbalimbali vya mpira.