Browsing: Video Mpya

Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) alipotembelea banda la wakala wa nishati vijijini, akiunga mkono juhudi za serikali katika kuhakikisha kuwa huduma za nishati zinawafikia wananchi wa maeneo ya vijijini na kusaidia maendeleo yao ya kiuchumi.

Vilevile, kampeni hii inapata sapoti kubwa kutoka kwa Rais Samia Suluhu Hassan, ambaye ameonyesha dhamira yake ya dhati ya kuleta mabadiliko katika maisha ya wanawake na wananchi wa maeneo ya vijijini. Rais Samia amesisitiza umuhimu wa ushirikiano na maendeleo endelevu katika kuhakikisha kuwa haki na fursa sawa zinapatikana kwa wote, hususan wanawake, katika kukuza uchumi wa taifa letu.”

Hii inaonyesha mchango mkubwa wa Rais Samia katika kuhamasisha mabadiliko chanya, hasa kwa wanawake, kupitia kampeni ya Nishatisafi na kuhakikisha kwamba huduma za kimsingi kama nishati zinawafikia wananchi wa vijijini.

Umoja wa Machinga wa eneo la Old Airport katika Jiji la Mbeya wamemchangia Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Dkt. Tulia Ackson, kiasi cha shilingi milioni moja (1,000,000/=) ili aweze kuchukua fomu ya kugombea Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), kufuatia chama hicho kutangaza tarehe rasmi za kuchukua fomu.

Fedha hizo zimekabidhiwa kwa Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya, Dormohamed Issa, ambaye alimwakilisha Dkt. Tulia katika hafla hiyo ya makabidhiano.