Browsing: Video Mpya

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb), amempongeza Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson, kwa uongozi wake wa mfano unaoleta mageuzi chanya kupitia Mbeya Tulia Marathon.

Akizungumza Mei 10, 2025 katika Uwanja wa Sokoine, Mbeya, mara baada ya kushiriki mbio fupi za Tulia Marathon, Mhe. Mahundi alisema kuwa mashindano hayo si tu ni burudani ya michezo bali pia ni jukwaa la kugusa maisha ya Watanzania wengi kupitia uboreshaji wa huduma za afya, elimu na kusaidia makundi yenye uhitaji.

“Spika Tulia si kiongozi tu wa kitaifa, bali ni dira ya matumaini kwa jamii. Kupitia Mbeya Tulia Marathon ameonyesha kuwa michezo ni daraja la maendeleo,” alisisitiza Mhe. Mahundi.

Mashindano haya yameendelea kuthibitisha kuwa michezo inaweza kuwa chachu ya mshikamano, afya bora, na maendeleo endelevu kwa taifa.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Mwaselela, amekabidhi vyerehani viwili kwa vijana wa Hamasa wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Mbeya Mjini ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuwawezesha kiuchumi na kuhamasisha uzalishaji wa ndani.

Akizungumza katika hafla fupi ya makabidhiano, MNEC Mwaselela alieleza kuwa msaada huo ni sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya chama ya kujenga vijana waadilifu, wachapakazi na wenye kujitegemea. Alisisitiza kuwa uwezeshaji wa vitendea kazi ni kichocheo muhimu katika kuleta maendeleo ya mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Viongozi wa UVCCM pamoja na wanachama walitoa shukrani kwa mchango huo na kuahidi kuvitumia vyerehani hivyo kwa malengo yaliyokusudiwa.