Browsing: Video Mpya

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kwa namna moja au nyingine kuna baadhi ya taasisi za dini zimejiingiza kwenye mkumbo ambao unaendelea wenye nia ovu ndani yake. Akieleza juu ya uongozi wa nchi katika kufuata misingi ya katiba na sheria, Rais Dkt. Samia amesema Tanzania haina dini lakini Watanzania wana dini za madhehebu mbalimbali huku akisisitiza kuwa kikatiba na sheria za nchi hakuna dini na dhehebu lolote lenye uwezo wa’kuover ride’ madhehebu mengine. Akizungumza na Wazee wa mkoa wa Dar es salaam leo tarehe 2 Disemba 2025, Rais DKt. Samia ameyasema na kuyasisitizia haya kuhusu taasisi za dini nchini “Viongozi wa dini msijivishe majoho ya kwamba nyinyi ndio mnaweza ‘kuover run’ nchi hii, hakuna. Tutakwenda kwa kwa Katiba na Sheria ya Nchi hii.” “Hatutaendeshwa na madhehebu yoyote ya dini, madhehebu ya dini na wafuasi wao” “ubora wa dini upo miyoyoni kwetu, wale wanaoamini ndio wanajua ubora wa dini yao..” “hakuna ‘over riding’ hapa! Kwamba “mimi dini yangu ndio itaover ride Tanzania na tamko nikilitoa ndio hilo hilo”. “…hata wenyewe wanatofautiana, mimi toka nimekaa matamko 8 yametolewa na TEC, lakini ukienda chini chini wenyewe wanapingana, matamko yale hayafanyi kazi…waliosimama kwenye mstari wa haki wanaona ni batili iliyofanyika..hawaungani nao..” “Tanzania yetu ni nchi ya umoja na mshikamano, amani na utulivu ndio ngazo zetu, tusivurugwe ndugu zangu

*SAFARI YENYE TABASAMU KATA YA ILEMI.*

Kazi inaendelea pale ilipoishia katika kusambaza Tabasamu Kwa Wananchi wa Jimbo la Uyole Ndani ya kata Ya Ilemi Mkoani Mbeya.

Familia ya Anyomwisye Mwalyaje inaenda Kutabasamu, hii ni baada ya kukutana na changamoto ya nyumba ambayo walikuwa wakiishi kupata ajali ya Moto Septemba 05, 2025.

Kama kawaida ya Taasisi ya Tulia Trust chini ya mkurugenzi wake ambae ni Mbunge Jimbo la Uyole na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani(IPU) Mh. Dkt. Tulia Ackson imedhamiria kurudisha Tabasamu Kwa familia hiyo.

@tuliatrust_tz
@tulia.ackson

#TuliaTrustNaJamii
#TabasamishaNaTuliaTrust
#TuliaTrustMtaaniKwetu

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Mhe. Patrick Mwalunenge, ameendelea kuwawezesha vijana wa bodaboda jijini Mbeya kwa kutoa msaada katika vijiwe mbalimbali.

Katika ziara hiyo, ametoa bodaboda moja kwa vijana wa kijiwe cha Nzovwe, pamoja na mtaji wa mafuta wa shilingi 40,000 kwa kila kikundi alichotembelea. Aidha, ameacha shilingi 400,000 kwa ajili ya kuwaendeleza vijana wengine.

Mhe. Mwalunenge amewahimiza vijana kuwa watulivu na wavumilivu wakati serikali ikiendelea kuweka mikakati madhubuti ya kuwawezesha kupitia fursa za kiuchumi.