Browsing: Video Mpya

Rais wa Mabunge Duniani (IPU), Dkt. Tulia Ackson anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa kitabu Ndoto ya Yatima kilichoandikwa na Shukurani Gideon Mwasanjobe, Mkurugenzi wa Tehla Foundation (TEFO) na mmiliki wa Shule ya Sekondari Vanessa. Uzinduzi huo utafanyika Septemba 13, 2025 jijini Mbeya.

Kwa kaulimbiu “Tambua Thamani ya Ndoto Iliyojificha Ndani ya Yatima”, kitabu hiki kinalenga kuibua ari na matumaini kwa watoto yatima. Mratibu wa tukio, George Mwaitenda, amesema uzinduzi huo utahusisha ushuhuda kutoka kwa watoto waliowahi kunufaika na malezi ya taasisi za TEFO na Shury Agri Farm Ltd.

Zephania Gideon Kang’anga, Mkurugenzi wa Shury Agri Farm Ltd, amesema taasisi yao kwa kushirikiana na TEFO inalenga kusaidia watoto yatima kutambua na kutimiza ndoto zao kupitia elimu na ujasiriamali.

Kwa upande wake, Katibu wa Asasi za Kiraia Jiji la Mbeya, Mustafa Namnenje, amepongeza juhudi za Mwasanjobe kuwekeza katika maisha ya watoto yatima, huku akiitaka jamii kuunga mkono jitihada hizo.

Mwalimu Andrew Ezekiel Wihala, mlezi wa watoto yatima, amesisitiza kuwa tukio hilo lina umuhimu wa kijamii kwani linawakumbusha Watanzania wajibu wa kuwatunza na kuwawezesha watoto waliopoteza walezi wao.

Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi, Emmanuel Mwambelo, pamoja na Benson Thom na Deborah Emmanuel, wamezitaka taasisi na wadau kuunga mkono na kudhamini tukio hilo la kihistoria litakalogusa maisha ya we

Wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya Kata jijini Mbeya wametakiwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ya uchaguzi ili kuepusha vurugu wakati wa mchakato wa uchaguzi mkuu.

Tahadhari hiyo imetolewa na Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo, Anamary Joseph, anayesimamia majimbo ya Mbeya Mjini na Uyole, wakati wa mafunzo kwa wasimamizi wa uchaguzi wa kata hizo.

Afisa Uchaguzi wa Jiji la Mbeya, Gregory Emmanuel, amesisitiza umuhimu wa wasimamizi hao kuwa na nyaraka muhimu kama Katiba na kanuni za uchaguzi ili kusimamia kikamilifu utoaji na urejeshaji wa fomu za wagombea pamoja na ratiba ya kampeni.

Washiriki wa mafunzo hayo wameonesha utayari wao kutekeleza majukumu kwa weledi ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu

Serikali imezindua mkakati wa kuongeza fursa za ardhi kwa vijana kupitia Benki Maalum ya Ardhi, taasisi itakayowezesha vijana kumiliki maeneo kwa ajili ya kilimo, ujenzi na uwekezaji.Katika ufunguzi wa maonesho ya kilimo Nane Nane mkoani Mbeya, Mkuu wa Mkoa Beno Malisa amesisitiza umuhimu wa vijana kuondokana na changamoto za ardhi na kutumia pembejeo bora ili kuongeza tija kwenye kilimo.Aidha, Meneja wa Azania Bank Mkoa wa Mbeya ameahidi kuunga mkono jitihada hizo kwa kuwapatia wananchi huduma rafiki za kifedha zitakazowezesha maendeleo katika kilimo na ufuga

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, Dkt. Godlove Mbwanji, kwa kushirikiana na Makamu wa Rais wa taasisi ya Smile Train Afrika, Bi. Nkeiruka Obi, leo Agosti 1, 2025, wamezindua rasmi chumba cha upasuaji kwa watoto kilichokarabatiwa na kuwekewa vifaa vya kisasa.

Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Mbwanji amesema chumba hicho kina mazingira rafiki na ya kuvutia kwa watoto, hatua itakayosaidia kupunguza hofu na kuongeza furaha kwa watoto wanaohitaji huduma za upasuaji.

Kwa upande wake, Bi. Obi amesema Smile Train imekuwa ikitoa huduma nchini tangu mwaka 2006, ambapo zaidi ya watoto 15,000 wamenufaika na mafunzo kutolewa kwa zaidi ya wahudumu wa afya 1,000.

Dkt. Amosi Zakaria, Daktari Bingwa wa Usingizi kwa watoto, ameishukuru Smile Train kwa kufanikisha ukarabati huo na kusema sasa wanaweza kufanya upasuaji mkubwa kwa watoto wa umri wowote.

Tangu kukamilika kwa ukarabati huo, tayari watoto 210 wamefanyiwa upasuaji.