Browsing: Video Mpya

Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mbeya (MBEYAUWSA) imefuta madeni ya wateja wa kata ya Mwasenkwa waliokuwa wakitumia mradi wa maji wa kijiji na kushindwa kulipa ankara kwa muda mrefu.

Uamuzi huo umetangazwa wakati wa uzinduzi wa mradi mpya wa kisima kirefu chenye uwezo wa kuzalisha lita 720,000 za maji kwa siku, utakaohudumia wakazi zaidi ya 2,800. Mradi huu unaleta huduma ya maji kwa masaa 24.

Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya Mjini, Dkt. Tulia Ackson, alizindua mradi huo na kuhimiza wananchi kupanda miti rafiki kwa vyanzo vya maji ili kukabiliana na mahitaji yanayoongezeka.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 18 Aprili 2025, ameongoza wananchi wa Jiji la Mbeya katika zoezi la upimaji na matibabu ya macho.

Zoezi hilo limeanza rasmi leo katika Shule ya Msingi Kagera, iliyopo Kata ya Ilomba na litadumu kwa siku tatu mfululizo. Huduma hiyo ya afya ya macho inatolewa bila malipo kupitia Taasisi ya Tulia Trust kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa afya.

Katika hotuba yake, Dkt. Tulia amewasihi wananchi wa Mbeya kujitokeza kwa wingi ili kunufaika na huduma hizo muhimu kwa afya zao, akisisitiza dhamira ya Taasisi ya Tulia Trust katika kuboresha ustawi wa jamii kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo.

Mbeya, Tanzania – Aprili 2025
Wakazi wa maeneo ya Mwansekwa na Igodima jijini Mbeya wameeleza furaha yao kufuatia kuboreshwa kwa huduma ya upatikanaji wa maji safi katika maeneo yao, hali ambayo ni tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

Wananchi hao wameipongeza Serikali pamoja na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya (MBEYA-UWSA) kwa juhudi walizozifanya kuhakikisha wanapata huduma ya maji kwa uhakika. Wamesema kuwa huduma hiyo imeleta unafuu mkubwa katika maisha yao ya kila siku, hasa kwa upande wa wanawake na watoto waliokuwa wakitembea umbali mrefu kutafuta maji.

“Kwa sasa tunapata maji karibu kabisa na nyumbani, tofauti na zamani tulipokuwa tukiteseka,” alisema mmoja wa wakazi wa Mwansekwa.

Kwa upande wake, MBEYA-UWSA imeeleza kuwa maboresho hayo ni sehemu ya mpango wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kuboresha huduma za maji mijini na vijijini kwa kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanapata huduma hiyo muhimu kwa maendeleo na ustawi wa jamii.