Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- DED Yegella: Ahamasisha Upigaji Kura, Kamanda Kuzaga Asema Jeshi la Polisi Lipo Tayari Kulinda Amani
- RC Malisa Atoa Wito wa Kulipa Leseni Wakati Akikabidhi Madawati 1,000 kwa Shule 15 Jijini Mbeya
- ISAACK MWAKIBOMBAKI MGOMBEA UDIWANI KATA RUANDA MBEYA AELEZA DHAMIRA YAKE KWA WAKAZI WA RUANDA
- Kijana Asiyeamini Katika Bahati Anashangaza Wote Baada ya Kushinda Kiasi Kikubwa Kwenye Bet
- Nilivyopata Flat Tummy Baada ya Kuteseka na Kitambi kwa Miaka Mitatu
- Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Beno Malisa Atoa Rai ya Kudumisha Amani Kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 29
- MKONGOMAN ATOA USHUHUDA MZITO KUTOWEKA KWA AMANI NCHINI JAMHURI YA KONGO
- DKT HARRISON MWAKYEMBE ATOA SOMO ZITO KUELEKEA UCHAGUZI MKUU
Browsing: Video Mpya
Zaidi ya wanaume 1000 kutoka katika mji wa Tunduma mkoani Songwe wamefunga Barabara kwa saa kadhaa wakifanya matembezi ya aina yake na kuwaacha watu midomo wazi barabarani wakiadhimisha mwaka mmoja wa muungano wa kikundi chao maalum Cha kijamii chenye lengo la kuinuana na kusaidiana wao kwa wao.
Mwenyekiti wa kikundi hicho Herode Jivava anasema waliamua kuanzia kikundi hicho ili kumkomboa mwanaume na aibu ambazo amekuwa akikumbana nazo pindi linapotokea jambo la furaha ama huzuni hivyo wao wapo kwaajili ya kumuinua na kumrejeshea heshima mwanaume huyo.
Mbeya, Septemba 28, 2025 – Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limefanikisha operesheni maalum iliyopelekea kuuawa kwa watuhumiwa waliodaiwa kuhusika na utekaji na mauaji ya kikatili ya Shyrose Michael Mabula [21], mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu cha Mzumbe Ndaki ya Mbeya, Kitivo cha Sheria.
Shyrose aliripotiwa kutekwa nyara Septemba 14, 2025 na mwili wake kupatikana Septemba 16 usiku katika Mtaa wa Morovian, Kata ya Isyesye Jijini Mbeya ukiwa umechomwa moto. Uchunguzi uliofanywa na Polisi uliwakamata watuhumiwa watatu: Marwa Nyahega John [25], Edward Christopher Kayuni, na Websta William Mwantebele [27], ambao walikiri kupanga njama za kumteka kwa lengo la kujipatia fedha kutoka kwa baba yake, Dkt. Mabula Michael.
Kwa mujibu wa Polisi, baada ya kushindikana kwa mpango huo, walimnywesha sumu ya kuulia magugu aina ya Round Up bila mafanikio, kisha wakamnynonga kwa kamba na kuuchoma moto mwili wake.
Mnamo Septemba 27, 2025, wakati wa operesheni katika Kijiji cha Chalangwa, wilayani Chunya, watuhumiwa Edward na Websta walijaribu kukimbia na kuwashambulia askari kwa kisu. Polisi walifyatua risasi za tahadhari, lakini walipokaidi amri, walijeruhiwa kwa risasi na kufariki dunia wakipelekwa hospitalini. Mtuhumiwa wa tatu, Marwa, naye alifariki baada ya kujirusha kutoka kwenye gari la Polisi wakati akipelekwa kuonyesha vielelezo.
Katika upekuzi, Polisi walipata pingu mbili, vitambulisho feki vya JWTZ, simu zenye picha za utekaji na mawasiliano yao, pamoja na taarifa kwamba kidole na nguo za marehemu vilikuwa vimepelekwa kwa mganga wa jadi kwa ajili ya zindiko. Mganga huyo kwa sasa anatafutwa.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeonya vijana na wananchi kwa ujumla kuacha tamaa ya mali kwa njia za haramu, na kusisitiza kuwa uhalifu haulipi na mkono wa sheria utawafikia popote pale.
Imetolewa na:
Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Mbeya
Mgombea Udiwani Kata ya Chokaa Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya Joshua Mlambalala amefikisha maombi ya minara ya mawasiliano kwa Kijiji cha Mapogolo Kata ya Chokaa mbele ya Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Maryprisca Mahundi Mbunge mteule wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya kutokana na umuhimu mkubwa kibiashara hasa Wachimbaji wa madini ya dhahabu eneo hilo.
Mlambalala amefikisha kilio hicho kwenye kampeni za Urais, Ubunge na Udiwani kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) zilizofanyika Kata ya Chokaa mgeni rasmi akiwa ni Mhandisi Maryprisca Mahundi.
Akijibu maombi hayo Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema suala hilo lipo ndani ya uwezo wake hivyo anawaagiza wataalam haraka iwezekanavyo ili kuwaondolea kadhia wananchi wa Mapogolo.
Akiomba kura Urais, Ubunge na Udiwani Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan imefanya maendeleo makubwa hivyo kuna kila sababu ya kukipa kura Chama Cha Mapinduzi.
Aidha amesema wananchi wajitokeze kupiga kura kumchagua Masache Kasaka nafasi ya Ubunge na Joshua Mlambalala nafasi ya Udiwani ili kutimiza mafiga matatu kwa maendeleo ya Kata,Wilaya na nchi kwa ujumla.
Uchaguzi mkuu utatamatisha oktoba 29 mwaka huu ambapo Mhandisi Maryprisca Mahundi ameendelea kuomba kura maeneo mbalimbali nchini.
Mbunge mteule wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi ameibukia Soko la Uhindini lililopo Kata ya Chokaa Wilaya ya Chunya Mkoani kwa lengo la kukutana na Wanawake wajasiriamali wanaofanya biashara katika Soko hilo.
Aidha amewatia moyo na kuwahimiza kumiliki uchumi wao sanjari na kujiunga pamoja ili waweze kunufaika na mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Halmashauri.
Aidha Mahundi ametumia fursa hiyo kuzisaka kura za Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, Mbunge na Diwani ili kuendeleza maendeleo nchini.
Leo nimekuja mbele yenu nikiwa na ari na msisimko wa kweli. Nitumieni nikafanye kazi kwa ajili yenu na kwa ajili ya maendeleo ya Jimbo la Mbeya Mjini.
Nataka tushirikiane kubadilisha Mkoa wa Mbeya – tubebe pamoja ajenda ya maendeleo kwa tabasamu na mshikamano. Nina afya, nina nguvu, nina ujuzi na ubunifu. Nina dhamira thabiti ya kusimamia na kulinda maslahi ya wananchi wa Mbeya.
Nikiwa mgombea wa Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), naomba tushirikiane katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29. Naomba kura zenu kwa ajili ya Rais wetu mpendwa, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kura kwa ajili yangu kuwa Mbunge wenu, na kura kwa Diwani wa CCM.
Tukiwa pamoja, tutaendelea kusonga mbele. Nitumieni nikafanye kazi.
Asanteni sana.
