Browsing: Video Mpya

Mbunge Mteule wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya, Mh. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amezindua kampeni za CCM Kata ya Mbugani, Wilaya ya Chunya, ambapo aliwaomba wananchi kumpa kura za heshima Mgombea Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mgombea Ubunge Jimbo la Lupa Masache Kasaka na Mgombea Udiwani Bosco Mwanginde. Mahundi alisema Dkt. Samia ni kiongozi shupavu aliyeendeleza miradi ya awamu ya tano na kuanzisha mipya kwa manufaa ya wananchi. Naye Bosco Mwanginde aliwashukuru wanachama kwa kumchagua na kuwataka kushirikiana naye katika kuwaletea maendeleo.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa, ametangaza kuwa Mkoa wa Mbeya umepewa heshima kubwa ya kuwa mwenyeji wa maadhimisho ya kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2025.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Mhe. Malisa amesema maandalizi yote ya sherehe hizo yanaendelea kwa kasi ili kuhakikisha Mkoa wa Mbeya unakuwa mwenyeji bora na unatimiza matarajio ya kitaifa.

Amesema sambamba na sherehe hizo, Mkoa wa Mbeya utakuwa na matukio mbalimbali ikiwemo:

Maonyesho ya Wiki ya Vijana yatakayofanyika kuanzia tarehe 08 – 13 Oktoba, 2025 katika Uwanja wa Soko la zamani Uhindini.

Misa Maalum ya Kumbukumbu ya Baba wa Taifa, Mwl. Julius Kambarage Nyerere itakayoadhimishwa tarehe 14 Oktoba, 2025 katika Kanisa Katoliki la Mwanjelwa.

Kupokelewa kwa Mwenge wa Uhuru utakaopokelewa na Mkoa wa Mbeya kutoka Mkoa wa Songwe kuanzia tarehe 07 – 13 Oktoba, 2025.

Sherehe za Kilele cha Kitaifa cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, zitakazofanyika tarehe 14 Oktoba, 2025.

Wito kwa Wananchi na Wadau

Mhe. Malisa ametoa wito kwa wananchi wote wa Mkoa wa Mbeya kujitokeza kwa wingi kushiriki sherehe hizo muhimu za kitaifa, hususan wakati Mwenge wa Uhuru unapita katika maeneo mbalimbali ya Mkoa.

Ameeleza kuwa ni muhimu wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya kilele ili kuujaza uwanja na kusherehekea tukio hilo la kihistoria.

Vilevile, ameyataka vyombo vya habari kuendelea kutoa taarifa kwa wananchi ili kudumisha mshikamano, amani na umoja katika Mkoa wa Mbeya na taifa kwa ujumla.

Aidha, amewataka wamiliki wa hoteli na nyumba za kulala wageni kuandaa maeneo ya malazi ya kutosha kwa wageni wote watakaoshiriki, huku akiwataka kutoongeza gharama za huduma hizo.

Wafanyabiashara wa vyakula na usafirishaji pia wamehimizwa kujipanga kwa ajili ya kutoa huduma bora kutokana na wingi wa wageni watakaofika Mbeya kwa ajili ya sherehe hizo.

Hitimisho

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa, amesisitiza kuwa Mkoa wa Mbeya umejipanga kikamilifu na upo tayari kwa heshima ya kuandaa kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2025.

“Mbeya ipo tayari kwa ajili ya kilele,” amehitimisha.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na uchunguzi wa tukio la
mauaji ya aliyekuwa Mwanachuo wa mwaka wa kwanza katika Chuo
Kikuu cha Mzumbe ndaki ya Mbeya kitivo cha sheria aitwaye Shairose
Michael Mabula [21].
Awali mnamo tarehe 14 Septemba, 2025 Baba mzazi wa marehemu
aitwaye Dkt Michael Mabula alifika kituo kikuu cha Polisi Mbeya na kutoa
taarifa ya kupotea kwa binti yake aitwaye Shairose Mabula ambapo
jalada la uchunguzi lilifunguliwa na kuanza ufuatiliaji ili kumpata. mnamo
tarehe 16 Septemba, 2025 saa 5:00 usiku huko Mtaa wa Morovian uliopo
Kata ya Isyesye Jijini Mbeya ilipokelewa taarifa ya ajali ya moto ambapo
Askari walifika eneo la tukio na kukuta kibanda kinateketea kwa moto.
Baada ya uchunguzi ilibainika kuna mwili wa mtu mmoja jinsia ya kike
unaugua ambaye kwa wakati huo hakuweza kutambulika.
Mwili wa marehemu ulichukuliwa na kuhifadhiwa Hospitali ya Rufaa
Kanda Mbeya na baada ya uchunguzi wa kitabibu na kuhusisha ndugu
ilibainika kuwa mwili huo ni wa Shairose Mabula aliyekuwa anatafutwa
baada ya kuripotiwa kupotea.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na uchunguzi wa kina
ikiwemo uchunguzi wa kisayansi ili kubaini na kutambua mwili wa
marehemu na kuwakamata waliohusika na mauaji haya. Aidha, Jeshi la
Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa yeyote mwenye taarifa
zitakazofanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa azitoe. Pia, Jeshi la Polisi
Mkoa wa Mbeya linaendelea kutoa rai kwa jamii kuacha tabia ya
kujichukulia sheria mkononi na kusababisha madhara makubwa kama
mauaji.
Imetolewa na:
Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa Mbeya.