Browsing: Video Mpya

*MBUNGE MASACHE AUNGURUMA NKUNG’UNGU*

Lupa 📍

Mbunge wa lupa-chunya *Mh Masache Kasaka* ameambatana na *Mh Juma Homera* mkuu wa mkoa wa mbeya katika ziara ya wilaya ya chunya lengo kubwa ni kusikikiliza kero za wananchi wa katika kata na vitongoji mbali mbali na kuzitafutia ufumbuzi.

Katika ziara hiyo *Mh Masache kasaka* amezungumza na wananchi hao na kupokea kero zao ikiwemo barabara itokayo mwanzo mgumu kuunganisha ngwala itafikishwa kwa *Mh Samia Suluhu* ili iweze kupatiwa ufumbuzi.

Sambamba na hilo *Mh Masache kasaka* ameshukuru serikali inayoongozwa na Rais *Mh Dkt Samia Suluhu* kwa namna alivyoweza kutekeleza miradi mbali mbali katika kata hiyo ya nkung’ungu na kuweka mabadiriko ambayo awali hayakuwepo.

*KAZI NA UTU*
*CHUNYA TUNASONGA MBELE*

*DKT. TULIA ATANGAZA KUGOMBEA JIMBO LA UYOLE*

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, ametangaza nia ya kugombea Ubunge katika jimbo jipya la Uyole mkoani Mbeya katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu.

Dkt. Tulia ametoa tamko hilo leo tarehe 23 Mei, 2025 alipokuwa akihutubia Mkutano Mkuu Maalum wa Wilaya ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambapo amesema kuwa ameamua kufanya uamuzi huo ili kuwahudumia wananchi wa Uyole kutokana na kasi ndogo ya maendeleo iliyopo katika eneo hilo.

“Maendeleo ya Uyole yanasonga kwa taratibu sana, nimeona ni vyema nijitoe kwa moyo wote kuhakikisha wananchi wa Uyole wanapata huduma stahiki na maendeleo ya haraka. Nitoe wito kwenu, watu wengi watakuja kwenu, chagueni kiongozi, chagueni mtumishi, itasaidia sana kuendelea kuyakimbiza maendeleo ya jamii,” amesema Dkt. Tulia.

TUNAMTAKA DKT TULIA AGOMBEE UYOLE SABABU YA MAENDELEO.

Wananchi wa maeneo mbalimbali katika Jimbo jipya la uyole wamemtaka mbunge wa Mbeya Mjini Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Mabunge duniani Dkt Tulia Akson kugombea jimbo la Uyole sababu ya utendaji mzuri wa kazi na kuleta maendeleo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumhiya ya vijana wa chama cha mapinduzi UVCCM wilaya ya Mbeya mjini Ameishukuru Tume ya uchaguzi kwa kuligawa jimbo hilo akieleza yakuwa kutakuwa na maendeleo ya Kasi katika Maeneo mbalimbali.