Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa saba [09] kwa tuhuma za utapeli na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kupitia mitandao ya kijamii ya Facebook na WhatsApp. Watuhumiwa hao walikamatwa kwa nyakati tofauti katika Misako inayofanywa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya ambapo Agosti 18, 2025 saa 6:00 mchana huko Kitongoji na Kata ya Nsalala, Tarafa ya Usongwe, walikamatwa watuhumiwa 04 wanaojishughulisha na utapeli wa fedha kupitia mitandao ya Facebook na WhatsApp kwa kudanganya wanatafuta wafanyakazi wa kuuza Supermarket iitwayo Kajala iliyopo Jijini Dar es salaam.
Watuhumiwa waliokamatwa ni Nemia Japhet Njonga [23] fundi rangi, mkazi wa mwakapangala, Ombeni Asangalwisye Ambilikile [22] Bodaboda, mkazi wa Nsalala, Jacob Peter Hamis [23] fundi rangi, mkazi wa mwakapangala, Baraka Joniphat Mgala [22] Bodaboda, mkazi wa mtaa wa Ndola Mbalizi.
Watuhumiwa wamekuwa wakitengeneza link za kughushi kwenye mitandao ya kijamii ya Facebook na WhatsApp ambapo mtu anayeomba ajira hutumia kujiunga kwenye kundi hilo na kisha hutumiwa ujumbe unaomtaka kutuma CV yake na kumuomba mtume fedha za kujaziwa fomu na kulipia sare za kufanyia kazi. Watuhumiwa wamekutwa wakiwa na simu mbalimbali pamoja na laini za simu za mitandao mbalimbali zilizosajiliwa kwa majina ya watu tofauti ambazo hutumika kupokelea fedha na kufanyia mawasiliano