Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100
- Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari
- VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII
- TAKUKURU MBEYA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 100, YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA
- Mfumo wa kidigitali wa Vyeti vya Uasili kupitia Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) waanza rasmi Machi 2, 2026
- MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA
- Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya
- Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato
Author: Mbeya Yetu
Shirika la Posta Tanzania (TPC) kupitia Ofisi yake ya Mkoa wa Mbeya, limeadhimisha Wiki ya Posta Duniani kwa kufanya shughuli za kijamii ikiwemo kukabidhi msaada wa vyandarua katika Hospitali ya Wilaya ya Igawilo, Jijini Mbeya. Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Meneja wa Shirika la Posta Mkoa wa Mbeya, Amos Millinga, alisema kuwa wiki hiyo imelenga kutoa elimu kwa wananchi kuhusu huduma mbalimbali za Posta, sambamba na kuadhimisha Siku ya Posta Duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka tarehe 9 Oktoba. “Wiki hii tumeendesha programu maalum inayolenga kutoa uelewa wa huduma zetu za Posta. Lakini sambamba na hilo, tunasherehekea Siku ya Posta Duniani…
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete akisalimiana na Meneja Mahusiano Idara ya Wateja Binafsi – Luiana Keenja, alipotembelea Banda la NMB kwenye Maadhimisho ya wiki ya Vijana katika viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya katikati ni Meneja Mauzo Kanda Nyanda za Juu Ungandeka Mwakatage. WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete ameipongeza Benki ya NMB kwa kuendelea kuwa karibu na Wananchi kwa kusogeza huduma kwa watu wa maeneo ya pembezoni. Kikwete ameongea hayo alipotembelea Banda la NMB kwenye Maadhimisho ya wiki ya…
Mkazi wa Mtaa wa Block “T” uliopo Kata ya Iyela Jijini Mbeya, Austack Mushi, ameomba Serikali ya Mkoa wa Mbeya kuingilia kati na kumsaidia kurejesha mali na fedha zake zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 100, baada ya kuvamiwa nyumbani kwake na watu wasiojulikana mnamo Septemba 30, mwaka huu.
TAARIFA KWA UMMA
ASHIKILIWA KWA TUHUMA ZA KUMUUA MAMA YAKE WA KAMBO
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Tatizo Yohana Mzumbwe, mkazi wa Masoko mkoani Mbeya kwa tuhuma za mauaji ya mama yake wa kambo aitwaye Merry Yohana [61] aliyekuwa mkazi wa Masoko kwa kumkata na panga kichwani.
Anatuhumiwa kutenda tukio hilo Oktoba 6, 2025 saa 2:00 asubuhi huko katika Kijiji cha Mapinduzi, Kata ya Masoko, Tarafa ya Isangati, Mkoani Mbeya, kwa kumuua Merry Yohana, ambaye pia alikuwa mkazi wa Masoko alikuwa mwenye ualbino.
Kufuatia tukio hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya lilianza msako mkali na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa majira ya usiku huko Kijiji cha Mapinduzi, Kata ya Masoko kuhusiana na tukio hilo.
Uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha tukio hilo ni mgogoro wa kifamilia kuhusu mashamba ambapo mtuhumiwa alikuwa akimshinikiza Merry Yohana [ambaye kwa sasa ni marehemu] kugawa mashamba ya urithi yaliyoachwa baada ya baba yake kufariki.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa baadhi ya vijana kuacha tamaa ya kutaka kujipatia mali kwa njia zilizo kinyume na sheria. Uchunguzi unakamilishwa ili hatua nyingine zichukuliwe dhidi ya mtuhumiwa kwa mujibu wa sheria.
Imetolewa na:
Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa Mbeya.
Leo kupitia kampeni ya GESI YENTE iliyoandaliwa na Oryx Gas Tanzania, washindi mbalimbali kutoka mkoa wa Mbeya wamekabidhiwa zawadi zao walizojishindia baada ya kushiriki kwenye kampeni hiyo.
Zawadi zilizotolewa ni pamoja na pikipiki, majiko ya gesi, baiskeli, helmeti, kofia, na zawadi nyingine nyingi — zote zikilenga kuwazawadia wateja waaminifu wa Oryx Gas wanaojaza mitungi yao kwa usalama na uhakika.
Kampeni hii maalum ya “Gesi Yente – Mambo ni Yente” ilizinduliwa tarehe 13 Agosti 2025 na itaendelea hadi 13 Oktoba 2025, ikitoa fursa kwa wateja wote wa Oryx Gas kujishindia zawadi kemkem kwa kujaza mitungi yao katika vituo rasmi vya kampuni hiyo.
💬 Oryx Gas Tanzania inawahamasisha wateja wote kuendelea kushiriki kampeni hii kwa kujaza mitungi yao ili nao wapate nafasi ya kujishindia zawadi kabla ya kampeni kumalizika.
🔥 Gesi Yente – Mambo ni Yente!
#OryxGas #GesiYente #MamboNiYente #Mbeya
Kampeni za Uchaguzi Mkuu zinaendelea kwa kasi katika Jimbo la Mbarali, ambapo Mgombea Ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa Bahati Keneth Ndingo, ameendelea na ziara yake ya kuomba kura kwa wananchi na wanachama wa CCM katika Kata ya Rujewa na maeneo ya jirani yanayo unda kata hiyo Katika ziara hiyo ya leo, Mhe. Bahati Ndingo ametembelea maeneo mbalimbali ya Kata ya Rujewa, yakiwemo maeneo ya: Ihanga, Luwilindi, Mkwajuni, Rujewa Mjini, Mabanda, na Ibara, ambapo amekuwa akizungumza moja kwa moja na wananchi, akiwasihi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025, na kuwachagua wagombea wote…
Leo 05 Oktoba 2025 Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mbarali kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Bahati Keneth Ndingo, ameendelea na kampeni zake za kishindo kwa kufanya ziara kubwa ya kampeni katika Kata ya Mahongole, akiinadi Ilani ya CCM kwa mwaka 2025. Mhe. Bahati Ndingo amepokelewa kwa shangwe na mamia ya wanachama na wapenzi wa CCM kutoka maeneo mbalimbali ya Kata ya Mahongole, hususan katika eneo la Igalako, ambako wananchi wamejitokeza kwa wingi kumsikiliza na sera za mgombea huyo Katika ziara hiyo, Mhe. Bahati Ndingo alipata nafasi ya kutembelea maeneo ya biashara, vijiwe vya bodaboda, pamoja na vilabu vya pombe…
Leo 04 Oktoba 2025 Mgombea Ubunge wa Jimbo la Uyole kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Tulia Ackson amesema kipaumbele kikubwa kwa sasa kwenye Sekta ya Afya Kata ya Mwansenkwa ni Kujenga Jengo la Mama na Mtoto pamoja na ukarabati wa Miundombinu kwenye Zahanati ya Kata hiyo. Akizungumza Mbele ya wakazi wa Mwansenkwa kwenye Mkutano wake wa Kampeni uliofanyika Mtaa wa Luala Dkt. Tulia amesema akipata ridhaa ya kuwaongoza Wananchi wa Jimbo la Uyole atahakikisha Jengo hilo linajengwa ili huduma ya Mama na Mtoto ipatikane jirani tofauti na ilivyo sasa. Sambamba na hayo amesema ataendelea na zoezi la…
