Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- Maelfu ya wana CCM Mbeya Wamiminika Songwe Kumlaki Dkt. Samia—Wavutiwa na Uongozi Wake wa Kipekee
- Nilivamiwa na Uchawi Kila Usiku Hadi Nilipopata Kinga Iliyowafanya Wachawi Washindwe Kunitazama Machoni
- TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI WA UDIWANI KATIKA KATA YA NYAKASUNGWA JIMBO LA BUCHOSA
- RC Malisa Azindua Wodi ya Watoto Wachanga Hospitali ya Meta Mbeya kwa Ushirikiano wa IHI na NEST360 Tanzania
- Nilivyolipizwa Kisasi na Aliyeniumiza Baada ya Kunitendea Vibaya, Sasa Anaomba Msamaha Kila Siku
- Nilivyomrudisha Mume Wangu Baada ya Miaka Mitatu ya Kuachana, Sasa Hachoki Kuniambia ‘You’re My Destiny
- Madaktari Walishangaa Nilivyopona Maradhi Ambayo Walikuwa Wamesema Hayatibiki
- Nilivyomfanya Mume Wangu Kusema ‘Baby Siwezi Tena’
Author: Mbeya Yetu
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele leo Septemba 21, 2025 ametembelea Halmashauri ya Mji wa Mafinga Wilayani Mufindi Mkoani Iringa ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kukagua maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 ambapo pamoja na mambo mengine alipokea taarifa ya Mji huo kutoka kwa wasimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri kuhusu maandalizi ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa Mwaka 2025 na kisha kukagua vifaa ambavyo tayari vimepokelewa katika Halmashauri hiyo. Jaji Mwambegele yupo Mkoani Iringa kukagua maandalizi hayo na kutazama kampeni za wagombea katika majimbo ya Mkoa…
Stephen Samuel Langeni, Mkurugenzi wa Maranatha Pharmacy na Maranatha Hospitali, ambaye pia ni Mwakilishi wa Wafanyabiashara Mkoa wa Mbeya, ametoa rai kwa viongozi na wananchi wa mkoa huo kushirikiana kulinda na kutunza rasilimali za kijani ambazo ndiyo fahari ya Mbeya. Akizungumza katika kikao maalum, Langeni alisema jina la Mbeya limekuwa likihusishwa moja kwa moja na mandhari ya kijani, lakini hali hiyo ipo hatarini kupotea kutokana na changamoto za ukataji miti holela pamoja na mwamko mdogo wa upandaji miti. “Mbeya imekuwa ikitambulika kama fahari ya kijani, lakini sasa sifa hii inaondoka kwa kasi kubwa. Kila siku miti mingi inakatwa, na hatua…
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele Septemba 19, 2025 ametembelea Halmashauri ya Jiji la Mbeya katika Majimbo ya Uchaguzi ya Mbeya Mjini na Uyole na kupokea taarifa ya mkoa kutoka kwa wasimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri zote za Mkoa wa Mbeya kuhusu maandalizi ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa Mwaka 2025 na kisha kukagua vifaa ambavyo tayari vimepokelewa katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya. Jaji Mwambegele pia alipata fursa ya kutembelea kampeni za wagombea Ubunge wa chama cha CUF na CCM katika majimbo hayo. Kwa mujibu…
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa, ametangaza kuwa Mkoa wa Mbeya umepewa heshima kubwa ya kuwa mwenyeji wa maadhimisho ya kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2025.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Mhe. Malisa amesema maandalizi yote ya sherehe hizo yanaendelea kwa kasi ili kuhakikisha Mkoa wa Mbeya unakuwa mwenyeji bora na unatimiza matarajio ya kitaifa.
Amesema sambamba na sherehe hizo, Mkoa wa Mbeya utakuwa na matukio mbalimbali ikiwemo:
Maonyesho ya Wiki ya Vijana yatakayofanyika kuanzia tarehe 08 – 13 Oktoba, 2025 katika Uwanja wa Soko la zamani Uhindini.
Misa Maalum ya Kumbukumbu ya Baba wa Taifa, Mwl. Julius Kambarage Nyerere itakayoadhimishwa tarehe 14 Oktoba, 2025 katika Kanisa Katoliki la Mwanjelwa.
Kupokelewa kwa Mwenge wa Uhuru utakaopokelewa na Mkoa wa Mbeya kutoka Mkoa wa Songwe kuanzia tarehe 07 – 13 Oktoba, 2025.
Sherehe za Kilele cha Kitaifa cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, zitakazofanyika tarehe 14 Oktoba, 2025.
Wito kwa Wananchi na Wadau
Mhe. Malisa ametoa wito kwa wananchi wote wa Mkoa wa Mbeya kujitokeza kwa wingi kushiriki sherehe hizo muhimu za kitaifa, hususan wakati Mwenge wa Uhuru unapita katika maeneo mbalimbali ya Mkoa.
Ameeleza kuwa ni muhimu wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya kilele ili kuujaza uwanja na kusherehekea tukio hilo la kihistoria.
Vilevile, ameyataka vyombo vya habari kuendelea kutoa taarifa kwa wananchi ili kudumisha mshikamano, amani na umoja katika Mkoa wa Mbeya na taifa kwa ujumla.
Aidha, amewataka wamiliki wa hoteli na nyumba za kulala wageni kuandaa maeneo ya malazi ya kutosha kwa wageni wote watakaoshiriki, huku akiwataka kutoongeza gharama za huduma hizo.
Wafanyabiashara wa vyakula na usafirishaji pia wamehimizwa kujipanga kwa ajili ya kutoa huduma bora kutokana na wingi wa wageni watakaofika Mbeya kwa ajili ya sherehe hizo.
Hitimisho
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa, amesisitiza kuwa Mkoa wa Mbeya umejipanga kikamilifu na upo tayari kwa heshima ya kuandaa kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2025.
“Mbeya ipo tayari kwa ajili ya kilele,” amehitimisha.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na uchunguzi wa tukio la
mauaji ya aliyekuwa Mwanachuo wa mwaka wa kwanza katika Chuo
Kikuu cha Mzumbe ndaki ya Mbeya kitivo cha sheria aitwaye Shairose
Michael Mabula [21].
Awali mnamo tarehe 14 Septemba, 2025 Baba mzazi wa marehemu
aitwaye Dkt Michael Mabula alifika kituo kikuu cha Polisi Mbeya na kutoa
taarifa ya kupotea kwa binti yake aitwaye Shairose Mabula ambapo
jalada la uchunguzi lilifunguliwa na kuanza ufuatiliaji ili kumpata. mnamo
tarehe 16 Septemba, 2025 saa 5:00 usiku huko Mtaa wa Morovian uliopo
Kata ya Isyesye Jijini Mbeya ilipokelewa taarifa ya ajali ya moto ambapo
Askari walifika eneo la tukio na kukuta kibanda kinateketea kwa moto.
Baada ya uchunguzi ilibainika kuna mwili wa mtu mmoja jinsia ya kike
unaugua ambaye kwa wakati huo hakuweza kutambulika.
Mwili wa marehemu ulichukuliwa na kuhifadhiwa Hospitali ya Rufaa
Kanda Mbeya na baada ya uchunguzi wa kitabibu na kuhusisha ndugu
ilibainika kuwa mwili huo ni wa Shairose Mabula aliyekuwa anatafutwa
baada ya kuripotiwa kupotea.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na uchunguzi wa kina
ikiwemo uchunguzi wa kisayansi ili kubaini na kutambua mwili wa
marehemu na kuwakamata waliohusika na mauaji haya. Aidha, Jeshi la
Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa yeyote mwenye taarifa
zitakazofanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa azitoe. Pia, Jeshi la Polisi
Mkoa wa Mbeya linaendelea kutoa rai kwa jamii kuacha tabia ya
kujichukulia sheria mkononi na kusababisha madhara makubwa kama
mauaji.
Imetolewa na:
Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa Mbeya.