Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- Mwanamke miaka 50 aoana na kijana wa miaka 21 baada ya penzi lao kuvutia kijiji kizima kwa mshangao
- KAILIMA AFUNGA KIKAO CHA UPANGAJI WA RATIBA YA KAMPENI ZA WAGOMBEA URAIS
- Pastor akimbia baada ya mke wake kuvamia madhabahu akilia
- MAHUNDI Atamka Hadharani: Samia na Tulia Ushindi wa Kishindo 2025
- Jinsi ya Kumkamata Mpenzi Wako Akiwa na Mpango wa Kando Bila Stress
- Masache Kasaka achukua fomu ya Ubunge Lupa Chunya aingia site kibabe
- MAHUNDI: CHAMA CHA MAPINDUZI NA MPEPERUSHA BENDERA MWALUNENGE NDIYO HABARI YA MBEYA MJINI
- “Nguvu ya Umoja: Mwakipesile Amuunga Mkono Patric Mwalunenge kuanzia Kampeni Hadi Ushindi”
Author: Mbeya Yetu
Rais wa Mabunge Duniani (IPU), Dkt. Tulia Ackson anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa kitabu Ndoto ya Yatima kilichoandikwa na Shukurani Gideon Mwasanjobe, Mkurugenzi wa Tehla Foundation (TEFO) na mmiliki wa Shule ya Sekondari Vanessa. Uzinduzi huo utafanyika Septemba 13, 2025 jijini Mbeya.
Kwa kaulimbiu “Tambua Thamani ya Ndoto Iliyojificha Ndani ya Yatima”, kitabu hiki kinalenga kuibua ari na matumaini kwa watoto yatima. Mratibu wa tukio, George Mwaitenda, amesema uzinduzi huo utahusisha ushuhuda kutoka kwa watoto waliowahi kunufaika na malezi ya taasisi za TEFO na Shury Agri Farm Ltd.
Zephania Gideon Kang’anga, Mkurugenzi wa Shury Agri Farm Ltd, amesema taasisi yao kwa kushirikiana na TEFO inalenga kusaidia watoto yatima kutambua na kutimiza ndoto zao kupitia elimu na ujasiriamali.
Kwa upande wake, Katibu wa Asasi za Kiraia Jiji la Mbeya, Mustafa Namnenje, amepongeza juhudi za Mwasanjobe kuwekeza katika maisha ya watoto yatima, huku akiitaka jamii kuunga mkono jitihada hizo.
Mwalimu Andrew Ezekiel Wihala, mlezi wa watoto yatima, amesisitiza kuwa tukio hilo lina umuhimu wa kijamii kwani linawakumbusha Watanzania wajibu wa kuwatunza na kuwawezesha watoto waliopoteza walezi wao.
Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi, Emmanuel Mwambelo, pamoja na Benson Thom na Deborah Emmanuel, wamezitaka taasisi na wadau kuunga mkono na kudhamini tukio hilo la kihistoria litakalogusa maisha ya we
Na Mwandishi Wetu Agosti 3, 2025 — Wazalishaji wa maudhui mtandaoni wametakiwa kuepuka kuchapisha taarifa zinazoweza kusababisha taharuki au kuchochea machafuko, hususan katika kipindi hiki kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika mwishoni mwa mwaka huu. Wito huo umetolewa na Meneja wa Kitengo cha Huduma za Utangazaji kutoka TCRA, Mhandisi Andrew Kisaka, alipokuwa akiwasilisha mada katika mkutano wa watoa maudhui mtandaoni ulioandaliwa na Tume Huru ya Uchaguzi (INEC). Mhandisi Kisaka amesema kuwa kipindi cha uchaguzi huwa na hali ya migawanyiko, mivutano na upotoshaji mkubwa, hivyo ni muhimu mabloga na watoa maudhui wengine kujiepusha kusambaza uvumi, kutangaza kwa umakini,…
Wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya Kata jijini Mbeya wametakiwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ya uchaguzi ili kuepusha vurugu wakati wa mchakato wa uchaguzi mkuu.
Tahadhari hiyo imetolewa na Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo, Anamary Joseph, anayesimamia majimbo ya Mbeya Mjini na Uyole, wakati wa mafunzo kwa wasimamizi wa uchaguzi wa kata hizo.
Afisa Uchaguzi wa Jiji la Mbeya, Gregory Emmanuel, amesisitiza umuhimu wa wasimamizi hao kuwa na nyaraka muhimu kama Katiba na kanuni za uchaguzi ili kusimamia kikamilifu utoaji na urejeshaji wa fomu za wagombea pamoja na ratiba ya kampeni.
Washiriki wa mafunzo hayo wameonesha utayari wao kutekeleza majukumu kwa weledi ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu
Arusha, Agosti 4, 2025 Tanzania imepewa heshima ya kuwa mwenyeji wa Warsha ya Wakuu wa Taasisi za Kuzuia na Kupambana na Rushwa kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), itakayofanyika kwa siku tatu kuanzia Agosti 4 hadi 6, 2025, katika Hoteli ya Gran Melia, jijini Arusha. Warsha hii ya kimataifa inafanyika wakati Tanzania ikiwa na jukumu la Uenyekiti wa Kamati ya Kupambana na Rushwa ya SADC (SADC Anti-Corruption Committee – SACC) kupitia Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), nafasi ambayo ilianza rasmi Oktoba 2, 2024. Hii ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya nchi…
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutanio wa Tume na Wazalishaji Maudhui Mtandaoni kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 03 , 2025. Baadhi ya wawakilishi wa serikali waliohudhuria mkutano huo. Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg.Kailima Ramadhani akitoa mada wakati wa ufunguzim wa mkutanio wa Tume na Wazalishaji Maudhui Mtandaoni kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo…
Serikali imezindua mkakati wa kuongeza fursa za ardhi kwa vijana kupitia Benki Maalum ya Ardhi, taasisi itakayowezesha vijana kumiliki maeneo kwa ajili ya kilimo, ujenzi na uwekezaji.Katika ufunguzi wa maonesho ya kilimo Nane Nane mkoani Mbeya, Mkuu wa Mkoa Beno Malisa amesisitiza umuhimu wa vijana kuondokana na changamoto za ardhi na kutumia pembejeo bora ili kuongeza tija kwenye kilimo.Aidha, Meneja wa Azania Bank Mkoa wa Mbeya ameahidi kuunga mkono jitihada hizo kwa kuwapatia wananchi huduma rafiki za kifedha zitakazowezesha maendeleo katika kilimo na ufuga
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutanio wa Tume na Waandishi wa Habari kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 02 , 2025. Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutanio wa Tume na Waandishi wa Habari kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 02 , 2025. …