Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- MWALUNENGE ATOA MILIONI 3 KUWAOKOA VIJANA WA KIWIRA BAADA YA TFS KUTAIFISHA VIFAA VYAO
- “MARUFUKU HUU UKAMATAJI TUMEKUBALIANA NA IGP” SIMBA CHAWENE
- WIZARA YA MAMBO YA NDANI YATOA ONYO MAANDAMANO KESHO/WAZIRI ATOA USHAURI KWA WANANCHI/MSIANDAMANE
- TANZANIA AND U.S. MOVE TO FINALISE MAJOR INVESTMENT AGREEMENTS
- “Hongera! Umeshinda JACKPOT ya Sh6,800,000”
- MFANYAKAZI WA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA APATA TUZO YA MWANAFUNZI BORA WA SHAHADA YA UZAMILI YA UDAKTARI WA MENO MUHAS.
- Ujumbe wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusu Maadhimisho ya Sikukuu ya Uhuru.
- Haikuwa tu safari ya kupona, bali safari ya kujikubali
Author: Mbeya Yetu
– Azungumza na vijana Tunduma, Mkoa wa Songwe Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Nanauka leo Novemba 25, 2025 amewasili mkoani Songwe kwa lengo la ziara ya kukutana na kuzungumza na vijana kuhusu masuala mbalimbali ya ustawi wa kundi hilo ikiwemo shughuli za Ajira, Uwezeshwaji kiuchumi, Elimu, Afya na Miundombinu kwa ajili ya ustawi wa maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla. Mhe. Waziri Nanauka ametembelea kwenye vijiwe pamoja na miradi ya vijana katika eneo la Sogea stendi, Kilimanjaro, Kisimani, Stendi ya zamani ya Majengo na Mpemba. Akizungumza mara baada ya kukutana na vijana…
Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe imezindua rasmi ujenzi wa Soko la Kisasa la Ndizi litakalogharimu Sh Bilioni 2.8, hatua inayotajwa kuwa mabadiliko makubwa katika sekta ya kilimo na masoko ya mazao wilayani humo. Akizungumza wakati wa utiaji saini wa mkataba huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Bw. Renatus Mchau, amesema Rungwe imechukua hatua ya kihistoria baada ya wananchi kusubiri kwa muda mrefu soko la uhakika la kuuza zao kuu la ndizi—zao ambalo limekuwa mhimili wa uchumi wa wilaya pamoja na mazao mengine kama kahawa, kakao, parachichi na viazi. Mchau amesema soko la sasa, hususan la Kiwira, halikuwa na mazingira rafiki, jambo…
MAMIA WAMPOKEA DKT. SAMIA ARUSHA, ASISITIZA UMUHIMU WA AMANI NCHINI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amewashukuru wananchi wa Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro kwa imani kubwa waliyompatia katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, akiahidi kurejea tena Mkoani Arusha kutoa shukrani zake kwa wananchi.
Dkt. Samia amebainisha hayo leo Ijumaa Novemba 21, 2025 alipotua katika Uwanja wa ndege wa Kilimanjaro (KIA) na kuzungumza na mamia ya wananchi waliofika uwanjani hapo Kumpokea, akianza ziara yake ya siku mbili Mkoani Arusha.
Katika salamu zake Rais Samia amesisitiza kuhusu umuhimu wa amani kwa ustawi na maendeleo ya Watanzania, akisisitiza wananchi kutotoa fursa katika kuharibu amani na kuwasihi Wazazi na walezi kuzungumza na Vijana wao pia kuhusu umuhimu wa kutunza amani ya Tanzania.
“Niwashukuru sana kwa kuendelea kuiweka mikoa hii kuwa salama. Usalama upo, kazi zinaendelea na mambo yetu yote yanaendelea. Niwaombe sana amani pekee ndiyo tumaini letu, uhai wetu ni amani yetu sasa niwaombe sana tusitoe fursa ya kuharibu amani yetu.” Amesema Rais Samia.
Rais Samia pia ametoa wito kwa wazazi na walezi kuzungumza na watoto wao kuhusu amani, akisema anafahamu kuwa matukio ya uvunjifu wa amani ya Oktoba 29, 2025 Vijana wengi walifuata mikumbo, akisema ni muhimu kuilinda amani kwani masuala ya uvunjifu wa amani si masuala ya kufanyia majaribio nchini.
Rais Samia yupo Mkoani kwa ziara ya siku mbili ambapo kesho Jumamosi Novemba 22, 2025 anatarajiwa kutunuku Kamisheni na Shahada ya Sayansi ya Kijeshi kwa Maafisa wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli Mkoani Arusha.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameelekeza Jeshi la Polisi na Uhamiaji kuhakikisha wanamkamata na kuzuia hati ya kusafiria ya mkandarasi anayejenga mradi wa Kituo cha ukaguzi cha Pamoja kilichopo Muhalala mkoani Singida. Dkt. Mwigulu amesema kuwa mkandarasi huyo aliaminiwa na Serikali kwa kupewa ujenzi wa mradi huo wa kimkakati uliosimama kwa zaidi ya miaka nane tangu mwaka 2016. Mradi huo unaojengwa na kampuni ya Impresa di Costruzioni Ing. E. Mantovani S.p.A ulipaswa kukamilika mwaka 2018. Ametoa agizo hilo leo Ijumaa tarehe 21 Novemba, 2025 wakati alipokagua mradi huo katika ziara yake ya kikazi mkoani…
Diwani wa Kata ya Ilomba, Ndg. Noah Edson Mwakisu, leo amerejesha fomu za kuwania Umeya wa Jiji la Mbeya kupitia CCM. Akizungumza katika Ofisi za CCM Mbeya Mjini, Mwakisu alisema anagombea nafasi hiyo ili kulipa jiji mwelekeo mpya wa maendeleo, akisisitiza umuhimu wa uongozi wenye maono, ushirikiano na uwajibikaji.
Mwakisu alisema Mbeya ina fursa kubwa za kimaendeleo kutokana na mazingira na jiografia yake, hivyo inahitaji kiongozi anayeendana na mahitaji ya kizazi cha sasa, hususan vijana ambao ndio nguvu ya uchumi wa jiji. Aliomba sapoti na baraka za wananchi, akiahidi kulifanya jiji hilo mfano wa kuigwa endapo atapewa dhamana.
Kurejesha fomu hizo kunamweka rasmi katika kinyang’anyiro cha ndani ya CCM cha kuwania Umeya wa Jiji la Mbeya mwaka huu.
