Browsing: Video Mpya

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza kuwa Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utafanyika Jumatano, Oktoba 29, 2025.

✅ Vituo vya kupigia kura vitafunguliwa saa 1:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni.
✅ Vituo vya magereza vitafunguliwa saa 2:00 asubuhi hadi saa 9:00 alasiri.
✅ Kila mpiga kura anatakiwa kufika kituoni na kadi yake ya kupigia kura.
✅ Waliopoteza kadi wataruhusiwa kutumia NIDA, leseni au pasi ya kusafiria endapo jina lipo kwenye daftari la wapiga kura.

🗓️ Taarifa hii imetolewa na Ms. Anamary Joseph Mbunga, Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Mbeya Mjini – tarehe 19 Oktoba 2025.

Wanachama wa CCM kutoka Mbeya Mjini na Vijijini wamejitokeza kwa wingi katika Uwanja wa Ndege wa Songwe kumlaki Mgombea Urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akitokea mkoani Rukwa kuelekea Dar es Salaam.

Wanachama hao walikaa uwanjani tangu saa 1 asubuhi hadi jioni wakisubiri kwa hamasa kumuona kiongozi wao, wakisema wanavutiwa na siasa za hekima, upendo na maendeleo za Dkt. Samia.

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali imeendelea kuchukua hatua madhubuti za kuimarisha ustahimilivu wa Taifa dhidi ya majanga, kupitia utekelezaji wa sera, sheria, mikakati na miradi mbalimbali

Amesema kuwa hatua hiyo itasaidia kuendelea katika kujenga ustahimilivu wa jamii dhidi ya maafa, tutaokoa maisha, mali, na rasilimali za taifa letu.

Amesema hayo leo Jumatatu (Oktoba 13, 2025) wakati alipotoa tamko katika maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Kupunguza madhara ya maafa, katika ukumbi wa mikutano wa City Park Garden jijini Mbeya.