Browsing: Video Mpya

*DKT. TULIA ATANGAZA KUGOMBEA JIMBO LA UYOLE*

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, ametangaza nia ya kugombea Ubunge katika jimbo jipya la Uyole mkoani Mbeya katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu.

Dkt. Tulia ametoa tamko hilo leo tarehe 23 Mei, 2025 alipokuwa akihutubia Mkutano Mkuu Maalum wa Wilaya ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambapo amesema kuwa ameamua kufanya uamuzi huo ili kuwahudumia wananchi wa Uyole kutokana na kasi ndogo ya maendeleo iliyopo katika eneo hilo.

“Maendeleo ya Uyole yanasonga kwa taratibu sana, nimeona ni vyema nijitoe kwa moyo wote kuhakikisha wananchi wa Uyole wanapata huduma stahiki na maendeleo ya haraka. Nitoe wito kwenu, watu wengi watakuja kwenu, chagueni kiongozi, chagueni mtumishi, itasaidia sana kuendelea kuyakimbiza maendeleo ya jamii,” amesema Dkt. Tulia.

TUNAMTAKA DKT TULIA AGOMBEE UYOLE SABABU YA MAENDELEO.

Wananchi wa maeneo mbalimbali katika Jimbo jipya la uyole wamemtaka mbunge wa Mbeya Mjini Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Mabunge duniani Dkt Tulia Akson kugombea jimbo la Uyole sababu ya utendaji mzuri wa kazi na kuleta maendeleo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumhiya ya vijana wa chama cha mapinduzi UVCCM wilaya ya Mbeya mjini Ameishukuru Tume ya uchaguzi kwa kuligawa jimbo hilo akieleza yakuwa kutakuwa na maendeleo ya Kasi katika Maeneo mbalimbali.