Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- Mtoto wa Jenista Mhagama Aibua Hisia Kali, Asema Mama Yake Hana Deni
- RAIS SAMIA KWA UCHUNGU MSIBANI – ”TUTALIMISI TABASAMU LAKE –
- MADEREVA BODABODA MKOANI IRINGA WALAANI VITENDO VYA UVUNJIFU WA AMANI.
- MAHAFALI YA 23 YA TAASISI YA UHASIBU TIA KAMPASI YA MBEYA, RC MALISA AWAALIKA WAWEKEZAJI MKOANI MBEYA.
- Ilinde biashara dhidi ya husda na mikosi
- Fanya hivi kuvutia fursa mpya za kazi
- WASHINDI WA MAWAZO BUNIFU WANAZUONI TAASISI YA UHASIBIU TIA KUFANYA ZIARA YA KIMAFUNZO NJE YA NCHI
- “KUNUNA MWISHO – MWALUNENGE AWAPA MOTISHA VIJANA WA KIWIRA: PESA IPO, CHANGAMKIA FURSA”
Browsing: Video Mpya
Mbunge mteule wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi ameibukia Soko la Uhindini lililopo Kata ya Chokaa Wilaya ya Chunya Mkoani kwa lengo la kukutana na Wanawake wajasiriamali wanaofanya biashara katika Soko hilo.
Aidha amewatia moyo na kuwahimiza kumiliki uchumi wao sanjari na kujiunga pamoja ili waweze kunufaika na mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Halmashauri.
Aidha Mahundi ametumia fursa hiyo kuzisaka kura za Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, Mbunge na Diwani ili kuendeleza maendeleo nchini.
Leo nimekuja mbele yenu nikiwa na ari na msisimko wa kweli. Nitumieni nikafanye kazi kwa ajili yenu na kwa ajili ya maendeleo ya Jimbo la Mbeya Mjini.
Nataka tushirikiane kubadilisha Mkoa wa Mbeya – tubebe pamoja ajenda ya maendeleo kwa tabasamu na mshikamano. Nina afya, nina nguvu, nina ujuzi na ubunifu. Nina dhamira thabiti ya kusimamia na kulinda maslahi ya wananchi wa Mbeya.
Nikiwa mgombea wa Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), naomba tushirikiane katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29. Naomba kura zenu kwa ajili ya Rais wetu mpendwa, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kura kwa ajili yangu kuwa Mbunge wenu, na kura kwa Diwani wa CCM.
Tukiwa pamoja, tutaendelea kusonga mbele. Nitumieni nikafanye kazi.
Asanteni sana.
Mbunge Mteule wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya, Mh. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amezindua kampeni za CCM Kata ya Mbugani, Wilaya ya Chunya, ambapo aliwaomba wananchi kumpa kura za heshima Mgombea Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mgombea Ubunge Jimbo la Lupa Masache Kasaka na Mgombea Udiwani Bosco Mwanginde. Mahundi alisema Dkt. Samia ni kiongozi shupavu aliyeendeleza miradi ya awamu ya tano na kuanzisha mipya kwa manufaa ya wananchi. Naye Bosco Mwanginde aliwashukuru wanachama kwa kumchagua na kuwataka kushirikiana naye katika kuwaletea maendeleo.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa, ametangaza kuwa Mkoa wa Mbeya umepewa heshima kubwa ya kuwa mwenyeji wa maadhimisho ya kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2025.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Mhe. Malisa amesema maandalizi yote ya sherehe hizo yanaendelea kwa kasi ili kuhakikisha Mkoa wa Mbeya unakuwa mwenyeji bora na unatimiza matarajio ya kitaifa.
Amesema sambamba na sherehe hizo, Mkoa wa Mbeya utakuwa na matukio mbalimbali ikiwemo:
Maonyesho ya Wiki ya Vijana yatakayofanyika kuanzia tarehe 08 – 13 Oktoba, 2025 katika Uwanja wa Soko la zamani Uhindini.
Misa Maalum ya Kumbukumbu ya Baba wa Taifa, Mwl. Julius Kambarage Nyerere itakayoadhimishwa tarehe 14 Oktoba, 2025 katika Kanisa Katoliki la Mwanjelwa.
Kupokelewa kwa Mwenge wa Uhuru utakaopokelewa na Mkoa wa Mbeya kutoka Mkoa wa Songwe kuanzia tarehe 07 – 13 Oktoba, 2025.
Sherehe za Kilele cha Kitaifa cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, zitakazofanyika tarehe 14 Oktoba, 2025.
Wito kwa Wananchi na Wadau
Mhe. Malisa ametoa wito kwa wananchi wote wa Mkoa wa Mbeya kujitokeza kwa wingi kushiriki sherehe hizo muhimu za kitaifa, hususan wakati Mwenge wa Uhuru unapita katika maeneo mbalimbali ya Mkoa.
Ameeleza kuwa ni muhimu wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya kilele ili kuujaza uwanja na kusherehekea tukio hilo la kihistoria.
Vilevile, ameyataka vyombo vya habari kuendelea kutoa taarifa kwa wananchi ili kudumisha mshikamano, amani na umoja katika Mkoa wa Mbeya na taifa kwa ujumla.
Aidha, amewataka wamiliki wa hoteli na nyumba za kulala wageni kuandaa maeneo ya malazi ya kutosha kwa wageni wote watakaoshiriki, huku akiwataka kutoongeza gharama za huduma hizo.
Wafanyabiashara wa vyakula na usafirishaji pia wamehimizwa kujipanga kwa ajili ya kutoa huduma bora kutokana na wingi wa wageni watakaofika Mbeya kwa ajili ya sherehe hizo.
Hitimisho
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa, amesisitiza kuwa Mkoa wa Mbeya umejipanga kikamilifu na upo tayari kwa heshima ya kuandaa kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2025.
“Mbeya ipo tayari kwa ajili ya kilele,” amehitimisha.
